Saturday 28 June 2008


DAVID VILLA KUIKOSA FAINALI!
Mshambuliaji wa Spain, David Villa, ambae ndie anaongoza kwa kufunga magoli kwenye Fainali za EURO 2008, hatocheza mechi ya fainali dhidi ya Ujerumani baada ya kuumia musuli za pajani kwenye mechi ya Nusu Fainali ambayo Spain waliipiga Urusi 3-0.

**********************************************************************************
THURAM ana tatizo la moyo!

Veterani wa Ufaransa, Lilian Thuram, ambae aliiwakilisha Ufaransa EURO 2008 na kutangaza kung'atuka timu hiyo mara tu baada ya kutolewa nje ya mashindano hayo walipofungwa 2-0 na Italy, ametangaza ana ugonjwa wa moyo.
Thuram, mwenye umri wa miaka 36, ambae alikuwa kwenye harakati za kuhama Barcelona na kujiunga na PSG ya Ufaransa, amesema amegundulika na ugonjwa kama ule uliomuua kaka yake aliefariki akicheza mpira wa vikapu.
Thuram alianzia kucheza soka la kulipwa klabu ya Monaco mwaka 1990 na alihamia Italy mwaka 1996 alikochezea timu za Parma na Juventus kisha kujiunga na Barcelona mwaka 2006.
Thuram alieiwakilisha Ufaransa mara 142, na ambae ndie mwenye rekodi ya kucheza mechi nyingi timu hiyo, alinyakua Kombe la Dunia 1998 na EURO 2000 akiwa na Ufaransa.


No comments:

Powered By Blogger