Tuesday 24 June 2008

Chama cha Kandanda Ureno chakanusha ripoti zinazomhusu Scolari juu ya Ronaldo!
Jana usiku Chama cha Kandanda Ureno kimetoa taarifa kupinga kauli zilizosemekana zimetolewa na Meneja wa Timu ya Taifa ya Ureno Luiz Felipe Scolari anaeachia ngazi rasmi kazi hiyo na kujiunga na Chelsea tarehe 1 Julai 2008
Taarifa hiyo inatamka: "Luiz Felipe Scolari amekataa moja kwa moja kwamba alihojiwa au kutamka chochote kuhusu Ronaldo na uvumi wa kuihama klabu yake. Anasikitika sana kuhusishwa na uongo na uvumi huu ambao unatangazwa bila kuthibitisha ukweli uko wapi’’

No comments:

Powered By Blogger