Thursday 26 June 2008

FAINALI: GERMANY V SPAIN!


SPAIN WAIBUGIZA URUSI 3-0!


Uhispania wakicheza kandanda safi hasa baada ya kuingizwa nyota wa Arsenal Cesc Fabregas baada ya kutolewa David Villa katika dakika ya 34 na hasa kipindi cha pili waliwashindilia Urusi 3-0 magoli yote yakipatikana kipindi hicho cha pili.
Xavi alifunga bao la kwanza dakika ya 50 baada ya kazi nzuri ya Iniesta na Fabregas alimtengenezea vizuri Danny Guiza aliefunga bao la pili dakika ya 73. Na ni Fabregas tena aliepika bao la tatu katika dakika ya 82 lililofungwa na David Silva.
Ni ukweli kabisa alieleta ushindi ni Cesc Fabregas kwani ndie alieonekana dhahiri akiiunganisha timu kwa ubora wa hali ya juu kabisa!
Sasa Uhispania itakwaana na 'MASHINE YA KIJERUMANI' kwenye FAINALI hapo Jumapili uwanjani ERNST HAPPEL STADION mjini Vienna, Austria.
Russia: Akinfeev, Aniukov, Vasili Berezutsky, Ignashevich, Zhirkov, Semak, Zyryanov, Semshov (Bilyaletdinov 56), Saenko (Sychev 57), Pavluchenko, Arshavin.
Akiba: Gabulov, Malafeev, Yanbaev, Alexei Berezutsky, Adamov, Ivanov, Shirokov, Bystrov.
Kadi: Zhirkov, Bilyaletdinov.
Spain: Casillas, Sergio Ramos, Marchena, Puyol, Capdevila, Iniesta, Xavi (Alonso 69), Senna, Silva, Villa (Fabregas 34), Torres (Guiza 69).
Akiba: Palop, Reina, Albiol, Fernando Navarro, Santi Cazorla, Sergio Garcia, Arbeloa, Juanito, De la Red.
Magoli: Xavi 50, Guiza 73, Silva 82.
Watazamaji: 50,000
Refa: Frank De Bleeckere (Belgium).


No comments:

Powered By Blogger