Thursday 26 June 2008

NANI KUINGIA FAINALI KUPAMBANA NA ‘MASHINE YA KIJERUMANI’?
LEO: NUSU FAINALI- SPAIN V RUSSIA!
Andrei Arshavin wa Urusi ameibuka na kuwa lulu kwenye michezo ya EURO 2008 hasa baada ya kuiongoza Urusi kuibamiza Uholanzi 3-1 kwenye Robo Fainali na kuifungisha virago Sweden 2-0 kwenye mechi ya KUNDI D.
Kama leo, kwenye mechi ngumu ya Nusu Fainali dhidi ya Uhispania, atafanikiwa kuwa shujaa kwa kuiongoza Urusi kuingia fainali kupambana na ‘MASHINE YA KIJERUMANI’ basi, bila shaka, ataibuka na tuzo ya Mchezaji Bora wa EURO 2008.
Lakini wengi wanashangazwa mbona kabla ya michuano hii dunia ilikuwa haijamskia huyu nyota Andrei Arshavin mwenye miaka 27? Warusi wanajibu haraka kwamba kosa ni kuwa katika miaka ya hivi karibuni Urusi ilikuwa haina mafanikio kwenye mechi za kimataifa ingawa wao walimtambua Andrei Arshavin ni moto tangu yuko mdogo.
Leo Andrei Arshavin ana kibarua kikubwa kwani kwanza anakutana na Uhispania timu ambayo tayari ishaifunga Urusia kwenye michuano hii ilipobamizwa 4-1 kwenye mechi za makundi katika kundi lao KUNDI D ingawa Andrei Arshavin hakucheza mechi hiyo kwani alikuwa kafungiwa. Pili timu ya Uhispania imesheheni mastaa kama vile Torres, Villa, Fabregas nk ambao wanatambulika dunia nzima.
Vikosi vya timu hizi mbili havina majeruhi wala athari za kufungiwa wachezaji.
Refa kwenye mechi hii ni Mbelgiji Frank De Bleec
kere.

No comments:

Powered By Blogger