Tuesday 17 June 2008

Austria 0-1 Germany & Poland 0-1 Croatia
Goli alilofunga Michael Ballack kwa mpira wa adhabu limeipa ushindi Germany dhidi ya wenyeji wenza Austria na kuwafanya wakutane na Portugal kwenye ROBO FAINALI .
Croatia, ambao tayari walishatinga ROBO FAINALI na watakutana na Uturuki, washindi wa pili KUNDI A, waliwafungisha virago Poland kwa bao 1-0.
MECHI ZA LEO
KUNDI C=kundi la kifo!
UHOLANZI V ROMANIA
UFARANSA V ITALIA
NI KWELI KUNDI LA KIFO=angalia hesabu zake:
UHOLANZI washaingia ROBO FAINALI tena ni mshindi wa kwanza hivyo atacheza na mshindi wa pili KUNDI D [ama Sweden au Urusi].
ITALIA atasonga mbele ikiwa tu watatoka sare ya magoli na Ufaransa wakati huo huo Uholanzi iwafunge Romania. Wakitoka sare ya 0-0 na Ufaransa itabidi Uholanzi iwafunge Romania 3-0!
Mahesabu ni rahisi kwa Ufaransa: wao lazima wawafunge Italia ili wawe na matumaini japo kidogo ya kuingia ROBO FAINALI na wakati huo huo waombe Mungu Romania asishinde mechi yake na UHOLANZI!
JUU YA YOTE, UHAKIKA ni kwamba mmoja ama MABINGWA WATETEZI WA DUNIA, ITALIA, au, UFARANSA, WASHINDI WA PILI DUNIANI, yuko nje!
RATIBA ROBO FAINALI
ALHAMISI 19 JUNI: PORTUGAL V GERMANY
IJUMAA 20 JUNI: CROATIA V TURKEY
JUMAMOSI 21 JUNI: NETHERLANDS V D2 [ama Sweden au Urusi]
JUMAPILI 22 JUNI: SPAIN V C2 [ama Ufaransa, Italia au Romania]


No comments:

Powered By Blogger