Saturday 21 June 2008



Croatia 1-1 Turkey (1-3 penalti)
Uturuki itapambana na Ujerumani kwenye Nusu Fainali ya EURO 2008 baada ya kuitoa Croatia 3-1 kwa penalti kufuatia suluhu ya 1-1 baada ya mchezo wa dakika 120.
Ivan Klasnic aliifungia Croatia kwa kichwa zikiwa sekunde tu zimebaki za muda wa nyongeza lakini Mturuki Semih Senturk alisawazisha wakati Refa akiwa tayari kumaliza mpira.
Arda Turan, Semih na Hamit Altintop walifunga penalti za Uturuki.
Luka Modric, Ivan Rakitic walikosa penalti za Croatia na Kipa wa Uturuki Rustu aliakoa penalti ya mwisho iliyopigwa na Mladen Petric.
CROATIA: Pletikosa, Corluka, Robert Kovac, Simunic, Pranjic, Srna, Modric, Nico Kovac, Rakitic, Kranjcar (Petric 64), Olic (Klasnic 97).GOLI: Klasnic 119.
Turkey: Rustu, Altintop, Zan, Asik, Balta, Topal (Senturk 76), Sarioglu, Sanli, Turan, Kazim-Richards (Boral 61), Nihat (Karadeniz 117). KADI ZA NJANO: Sanli, Turan, Boral, Asik.
GOLI: Senturk 120.
WATAZAMAJI: 50,000
REFA: Roberto Rosetti (Italy).

No comments:

Powered By Blogger