Wednesday 18 June 2008

MATOKEO KUNDI D:
URUSI YATINGA ROBO FAINALI KUKUTANA NA UHOLANZI
RUSSIA 2 SWEDEN 0
SPAIN 2 UGIRIKI 1
Urusi imekamilisha timu zitakazocheza ROBO FAINALI baada ya kuiendesha mchakamchaka Sweden na kuibuka na ushindi wa 2-1 ingawa ingekuwa si ajabu kama wangeshinda hata goli 6 kwa jinsi walivyotawala mchezo.
Sasa Urusi watacheza na Uholanzi ROBO FAINALI.
Katika mechi nyingine ya kukamilisha ratiba tu Uhispania ambao ndio wanaongoza KUNDI D na tayari walikuwa washatinga Robo Fainali waliwapiga Ugiriki 2-1 timu ambayo ilikuwa ishaaga michuano hata kabla ya kuanza hii mechi yao ya mwisho.

Ratiba kamili ya ROBO FAINALI ni kama ifuatavyo: [mechi zote ni saa 3.45 usiku saa za bongo]

ALHAMISI 19 Juni
URENO V UJERUMANI
Basel, Switzerland
IJUMAA 20 Juni
CROATIA V UTURUKI
Vienna, Austria
JUMAMOSI 21 Juni
UHOLANZI v URUSI
Basel, Switzerland
JUMAPILI 22 Juni
SPAIN V ITALIA
Vienna, Austria

No comments:

Powered By Blogger