Wednesday 18 June 2008

Nasri akubali mkataba Arsenal
Arsenal wamefanikiwa kumsaini nyota chipukizi wa Ufaransa kiungo Samir Nasri kutoka klabu ya Marseille ya huko Ufaransa. Mchezaji huyo wa mwenye umri wa miaka 20 ambae wengi humwita Zinedine Zidane mpya inasemekana amesaini mkataba wa miaka minne. Nasri aliechezea Ufaransa mechi mbili EURO 2008 ndie aliepata tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi msimu uliopita kwenye ligi ya Ufaransa na vilevile Mchezaji Bora wa Mwaka kwenye klabu yake Marseille. Wataalam wanahisi ataziba vizuri pengo litaloachwa na Hleb ambae inasemekana yuko mbioni kuhama Arsenal.

No comments:

Powered By Blogger