Thursday 19 June 2008


Barcelona kuwatema Deco, Ronaldinho na Eto'o
Ronaldinho, Deco na Samuel Eto'o inaelekea wako njiani kuuzwa na Barcelona baada ya Kocha mpya Pep Guardiola kutamka wachezaji hao hawamo kwenye mipango yake ya kikosi chake cha msimu ujao.
Wachezaji wote watatu hawakucheza vizuri msimu uliopita na muda mrefu walikuwa majeruhi. Pia kulikuwa na dhana kwamba wote watatu hawajitumi ipasavyo, wanaendeleza starehe na kuleta migogoro miongoni mwa wachezaji wengine.

Inaelekea Meneja mpya alieteuliwa jana kumrithi Frank Rijkaard anataka kuanza na ukurasa mpya. Pep Guardiola alikuwa Mchezaji wa zamani wa Barcelona kwa kipindi kirefu ingawa hajawahi kuwa Meneja wa timu yeyote
Kuna tetesi nyingi kuwa wachezaji hao wataenda Italia na hata Uingereza hasa Klabu ya Chelsea ikitajwa hasa kwa Ronaldinho baada ya Mbrazil mwenzake Scolari kuukwaa Umeneja huko Chelsea.

No comments:

Powered By Blogger