Saturday 21 June 2008



MECHI YA LEO ROBO FAINALI:
UHOLANZI v URUSI

KIWANJA: St Jakob-Park, Basel, Switzerland
Kocha wa Uholanzi, Marco Van Basten, leo anategemewa kurudisha uwanjani kikosi chake 'kamili' baada ya kuwapumzisha wachezaji 9 waliocheza mechi mbili za kwanza kwenye mechi yao ya mwisho ya kundi waliyoifunga Romania 2-1.
Ruud van Nistelrooy, Andre Ooijer na Dirk Kuyt wanategemewa watarejea uwanjani.
Nao Warusi, wakiongozwa na Kocha Mholanzi, Guus Hiddink ambae aliiongoza Uholanzi mpaka ikafika Nusu Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1998, amekiri taifa lake la Uholanzi ni timu bora ingawa ameahidi Urusi kucheza kufa na kupona.
Katika mechi nane zilizopita ambzo timu hizi zimekutana Uholanzi ameshinda mara 4 na Urusi mara 2 huku mechi 2 zikiisha suluhu.
MECHI ZIJAZO:
Ratiba ni kama ifuatavyo: [mechi zote ni saa 3.45 usiku saa za bongo]
ROBO FAINALI
JUMAMOSI21 Juni
UHOLANZI v URUSI
Basel, Switzerland
JUMAPILI 22 Juni
SPAIN V ITALIA
Vienna, Austria
NUSU FAINALI

JUMATANO 25 JUNI
UJERUMANI V UTURUKI
ALHAMISI 26 JUNI
UHOLANZI/URUSI V SPAIN/ITALIA

No comments:

Powered By Blogger