
Watani wa jadi huko Marekani Kusini wameendelea kusuasua kwenye mechi za awali kutafuta timu nne zitakazoingia Fainali ya Kombe la Dunia 2010 zitakazochezwa Afrika Kusini walipotoka suluhu 0-0 mjini Belo Horizonte, Brazil.

Argentina walionekana kujihami ingawa walimtumia sana Messi kutafuta magoli ya kiujanja na kila wakati walijiangusha wakitegemea mpiga frikiki stadi Riquelme atawaokoa.
Timu zilikuwa:
BRAZIL
JULIO CESAR, MAICON, LUCIO [Kepteni], JUAN, ANDERSON [DIEGO dakika ya 34, dakika ya 79 akaingia DANIEL ALVES], GILBERTO, MINEIRO, GILBERTO SILVA, ADRIANO [FABIANO dakika ya 71], JULIO BAPTISTA, ROBINHO
ARGENTINA
ABBONDAN, COLOCCIN, BURDISSO, GAGO, HEINZE, ZANETTI [Kepteni], RICARDO [AGUERO dakika ya 68], RIQUELME [BATTAGLIA dakika ya 84], MASCHERANO, GUTIERREZ, MESSI [PALACIO dakika ya 90]
No comments:
Post a Comment