Thursday 19 June 2008

BRAZIL 0 ARGENTINA 0
Watani wa jadi huko Marekani Kusini wameendelea kusuasua kwenye mechi za awali kutafuta timu nne zitakazoingia Fainali ya Kombe la Dunia 2010 zitakazochezwa Afrika Kusini walipotoka suluhu 0-0 mjini Belo Horizonte, Brazil.
Brazil walikosa nafasi nyingi na watakayoijutia ni ile Robinho alipomtoka mpaka kipa Abbondan na akashindwa kutumia akili ya kucheza na wenzake.
Argentina walionekana kujihami ingawa walimtumia sana Messi kutafuta magoli ya kiujanja na kila wakati walijiangusha wakitegemea mpiga frikiki stadi Riquelme atawaokoa.
Timu zilikuwa:
BRAZIL
JULIO CESAR, MAICON, LUCIO [Kepteni], JUAN, ANDERSON [DIEGO dakika ya 34, dakika ya 79 akaingia DANIEL ALVES], GILBERTO, MINEIRO, GILBERTO SILVA, ADRIANO [FABIANO dakika ya 71], JULIO BAPTISTA, ROBINHO
ARGENTINA
ABBONDAN, COLOCCIN, BURDISSO, GAGO, HEINZE, ZANETTI [Kepteni], RICARDO [AGUERO dakika ya 68], RIQUELME [BATTAGLIA dakika ya 84], MASCHERANO, GUTIERREZ, MESSI [PALACIO dakika ya 90]

No comments:

Powered By Blogger