Friday 20 June 2008



MECHI YA LEO:
ROBO FAINALI: Croatia v Turkey
KIWANJA: Ernst Happel Stadion, Vienna, AUSTRIA


Mashabiki zaidi ya 100,000 wakilindwa na Polisi zaidi ya 4,600 wanategemewa kumiminka mjini Vienna, Austria kwa ajili ya pambano hili la Robo Fainali. Mji huu wa Vienna wapo Waturuki 60,000 wanaoishi humo na Wacroatia wapatao 16,000 hivyo imebidi ulinzi uwe mkali.
Uturuki watamkosa Kipa na Nahodha Volkan Demirel ambae amefungiwa kucheza baada ya kupewa kadi nyekundu katika mechi na Czech na nafasi yake itachukuliwa na veterani wa mechi 116 za Timu ya Taifa ya Utuki Rustu Recber mwenye miaka 35 ambae wengi tutamkumbuka jinsi alivyokuwa akijipaka rangi machoni kwenye mechi za Fainali za Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger