Wednesday 18 June 2008


France 0-2 Italy
Netherlands 2-0 Romania
Italy wametinga Robo Fainali kupambana na Spain baada ya kuwafunga na kuwatoa nje ya EURO 2008 Ufaransa.
Ufaransa walianza mechi ya jana kwa mikosi kwani mchezaji wao muhimu Franck Ribery aliumia vibaya goti kwenye dakika ya 7 na Eric Abidal alipewa kadi nyekundu dakika ya 25 kwa kumchezea rafu Luca Toni na hivyo kutoa penalti iliyofungwa na Andrea Pirlo. Nae Thierry Henry alibabatizwa na frikiki ya Daniele De Rossi na kusababisha bao la pili.
Ingawa Italia wako Robo Fainali na watacheza na Spain watawakosa wachezaji wawili muhimu sana kwenye mechi hiyo viungo Andrea Pirlo na Gennaro Gattuso ambao wanakosa mechi moja kwa sababu ya kuwa na kadi.
Katika mechi nyingine ya KUNDI C, magoli ya Klaas-Jan Huntelaar na Robin van Persie wa Uholanzi yaliwamaliza Romania na kuwatoa nje ya EURO 2008.
Uholanzi waliobadilisha wachezaji tisa katika mechi hiyo ya jana wameshinda mechi zao zote za KUNDI C.
MECHI ZA LEO:
saa 3.45 usiku:
KUNDI D
SPAIN V UGIRIKI
Hii ni mechi ya kukamilisha ratiba tu kwani SPAIN tayari wako Robo Fainali wakiwa washindi wa kwanza kundi hili na UGIRIKI imeshaaga EURO 2008.
URUSI V SWEDEN
Hii ni mechi ya kuamua nani anaingia Robo Fainali kukutana na UHOLANZI. Timu zote zina pointi sawa 3 ila SWEDEN ana ubora wa magoli. Hivyo suluhu itamfanya Sweden atinge Robo Fainali wakati URUSI hawana njia ila lazima washinde.
ROBO FAINALI
ALHAMISI 19 Juni
URENO V UJERUMANI
Basel, Switzerland
IJUMAA 20 Juni
CROATIA V UTURUKI
Vienna, Austria
JUMAMOSI 21 Juni
UHOLANZI v MSHINDI WA PILI KUNDI D [ama SWEDEN au URUSI]
Basel,
JUMAPILI 22 Juni
SPAIN V ITALIA
Vienna, Austria
NUSU FAINALI
JUMATANO 25 Juni
MSHINDI URENO/UJERUMANI V CROTIA/UTURUKI
Basel, Switzerland
ALHAMISI 26 Juni
MSHINDI UHOLANZI/D2 V SPAIN/ITALIA
Vienna, Austria
FAINALI
29 Juni
Vienna, Austria

No comments:

Powered By Blogger