Monday 16 June 2008

RONALDO V REAL:
KWA SASA, FIFA HAICHUKUI HATUA
Chama cha Soka Duniani, FIFA, kimetoa taarifa kuhusu malalamiko ya Manchester United juu ya Real Madrid kujaribu kumrubuni Ronaldo yaliyowasilishwa rasmi kwao wiki iliyopita.
Taarifa ya FIFA inasema: ‘Tunathibitisha tulipokea malalamiko rasmi ya Manchester United yanayohusiana na mchezaji Cristiano Ronaldo na klabu ya Real Madrid. Kufuatana na vielelezo tulivyopewa kwa sasa hakuna kitu kinachoonyesha mkataba umevunjwa. Kwa hiyo, kufuatana na taratibu, kwa sasa hakuna kesi itakayofunguliwa ila tumekitaka Chama cha Mpira cha Spain kimjulishe mwanachama wao Real Madrid kuhusu kuvunja sheria, kanuni na taratibu zinazohusisha uhamaji wa mchezaji’

No comments:

Powered By Blogger