Friday 20 June 2008



United - Ronaldo hauzwi

Taarifa iliyotolewa kwenye tovuti ya MAN UNITED imesema: "Kufuatia taarifa za vyombo vya habari leo kuhusu hatma ya Cristiano Ronaldo, Klabu imeona bora itoe msimamo wake. United hawatasikiliza ombi lolote la kumuuza mchezaji huyo. Ronaldo amehususishwa kila mara kuwa anahamia Real Madrid na klabu inasisitiza: HAUZWI."
Akizungumza baada ya Ureno kutolewa EURO 2008 kwa kipigo cha 3-2 na Ujerumani Ronaldo alisema: "Baada ya siku mbili au tatu ntazungumza kuhusu nini kinakuja. Ntazungumza na United. Ntajaribu kufikia makubaliano na tutaona nini kitakuja."

No comments:

Powered By Blogger