Saturday 29 August 2009

Chelsea 3 Burnley 0
Wakiwa nyumbani Stamford Bridge Chelsea leo wamepata ushindi wao wa 4 katika mechi zao 4 za Ligi Kuu msimu huu walipowafunga Wababe wa Manchester United na Everton, Burnley, Timu iliyopanda Daraja msimu huu, kwa mabao 3-0.
Bao la kwanza la Chelsea lilipatikana kabla tu ya mapumziko baada ya Drogba kupiga krosi ya chinichimi golini na mpira kuguswa na Carlisle wa Burnley na kisha kumparaza Anelka na kutinga wavuni.
Bao la pili lilifungwa na Ballack kwa kichwa baada ya krosi ya Lampard.
Ashley Cole akafunga bao la 3 kufuatia gonga kati yake na Lampard.
Vikosi:
Chelsea: Cech, Bosingwa, Carvalho, Terry, Ashley Cole, Essien, Ballack, Deco, Lampard, Anelka, Drogba.
Akiba: Hilario, Ivanovic, Mikel, Malouda, Kalou, Sturridge, Belletti.
Burnley: Jensen, Mears, Carlisle, Bikey, Jordan, Alexander, Blake, Elliott, McCann, Paterson, Steven Fletcher.
Akiba: Penny, Kalvenes, McDonald, Gudjonsson, Thompson, Guerrero, Eagles.
Refa: Mark Clattenburg (Tyne & Wear).

No comments:

Powered By Blogger