Wednesday 26 August 2009

UEFA SUPER CUP IJUMAA!!!!
NI FC BARCELONA v FC SHAKHTAR DONETSK huko Monaco!!!

Dro ya Makundi UEFA CHAMPIONS LEAGUE kesho!!!
Vizito wa UEFA na Klabu kubwa za Ulaya kuanzia siku ya Alhamisi watamiminika katika “Ka-nchi” cha Monaco ili kushuhudia Dro ya Timu 32 zinazowania UEFA CHAMPIONS LEAGUE zitakapogawanywa katika Makundi manne ya Timu 4 kila moja na kucheza kwa mtindo wa Ligi wa nyumbani na ugenini.
Mara baada ya Dro hiyo, siku hiyo hiyo Alhamisi, kutafanyika tamasha maalum la kutoa Tuzo za Wachezaji Bora wa Ulaya kwa msimu wa 2008/9 Tuzo zikipewa kwa Mchezaji Bora wa Ulaya pamoja na Kipa Bora, Mlinzi Bora, Kiungo Bora na Mshambuliaji Bora.
Siku ya Ijumaa kutakuwa na Dro ya Timu 48 zinazoshindania EUROPA LEAGUE kugawanywa kwenye Makundi ili wacheze mtindo wa Ligi.
Kisha jioni siki hiyo hiyo, katika Uwanja uitwao Stade Loius II kutafanyika pambano la kuwania UEFA Super Cup katika ya Bingwa wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE Barcelona ya Spain na Bingwa wa UEFA CUP Shakhtar Donetsk ya Ukraine.

No comments:

Powered By Blogger