Monday 27 September 2010

Rooney kuikosa mechi na Valencia
Manchester United imethibitisha kuwa Nyota wao Wayne Rooney hatasafiri na Kikosi chao kwenda Spain kucheza na Valencia Siku ya Jumatano kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI kwa sababu ana maumivu ya enka.
Rooney aliumia enka na kutolewa mapema Kipindi cha Pili katika mechi ya jana ya Ligi Kuu Man United ilipotoka sare 2-2 na Bolton Uwanja wa Reebok.
Rooney sasa anaungana na Mkongwe Ryan Giggs kuwa kwenye listi ya majeruhi.
Man United walianza mechi kwenye Kundi C la UEFA CHAMPIONS LIGI kwa kutoka sare 0-0 na Rangers Uwanjani Old Trafford na Valencia walianza kwa kishindo huko ugenini Uturuki kwa kuibamiza Bursapor mabao 4-0.
Kwenye Ligi huko Spain, Valencia ndio vinara wa La Liga.
Lampard kuzikosa mechi muhimu
Frank Lampard atazikosa mechi muhimu za Klabu yake Chelsea na pia za England kwa sababu hajapona vizuri baada kufanyiwa upasuaji kutibu ngiri.
Lampard, Miaka 32, alifanyiwa operesheni mwishoni mwa Agosti na awali ilitegemewa atakaa nje kwa Wiki mbili lakini sasa, baada ya kuwa nje kwa mwezi mzima, Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti amethibitisha atakuwa nje kwa Wiki mbili zaidi.
Kwa kuwa nje kipindi hicho atazikosa mechi za Chelsea dhidi ya Marseille hapo kesho, ile ya Arsenal Oktoba 3 na mechi ya England ya Euro 2012 na Montenegro hapo Oktoba 12.
MATOKEO LIGI ZA ULAYA:
Jumapili, Septemba 26
Serie A
Cesena 1 Napoli 4
Fiorentina 2 Parma 0
Catania 1 Bologna 1
Chievo Verona 0 SS Lazio 1
Sampdoria 0 Udinese 0
Palermo 2 US Lecce 2
As Bari 2 Brescia 1
Juventus 4Cagliari 2
La Liga
Real Mallorca 2 Real Socieda 0
Espanyol 1 Osasuna 0
Deportivo La Coruna 0 Almeria 2
Real Racing Santander 0 Getafe CF 1
Hercules CF 2 Sevilla FC 0
Atletico de Madrid 1 Real Zaragoza 0
German Bundesliga
VfL Wolfsburg 2 SC Freiburg 1
FC Kaiserslautern 0 Hannoverscher 1
French Ligi 1
Brest 1 Valenciennes 0
Toulouse FC 1 Lille OSC 1
Racing Club de Lens 0 Paris Saint-Germain 2

No comments:

Powered By Blogger