Saturday 2 October 2010

Wigan 2 Wolves 0
Katika mechi ya Ligi Kuu iliyoanza mapema leo, Wigan wakiwa nyumbani Uwanja wa DW wameweza kuwatungua Wolves mabao 2-0.
Wolves ilibidi wacheze Mtu 10 kuanzia dakika ya 11 baada ya Karl Henry kutandikwa Kadi Nyekundu na Refa Lee Mason kwa kumchezea rafu mbaya Jordi Gomez.
Hadi mapumziko ngoma ilikuwa 0-0 na ni Jordi Gomez alieipatia Wigan bao la kwanza dakika ya 64 kwa frikiki murua.
Hugo Rodallega alipachika bao la pili dakika ya 85 baada ya kupokea pasi kutoka kwa Charles N’Zogbia.

No comments:

Powered By Blogger