Sunday 26 September 2010

Bolton 2 Man United 2
Leo huko Uwanja wa Reebok nusura Manchester United yawakute yale yaliyowakuta Chelsea na Arsenal hapo jana baada ya Vigogo hao wawili kufungwa lakini Manchester United walibahatika kwa kusawazisha mara mbili baada ya Bolton kuchukua uongozi mara mbili.
Zat Knight ndie alieipatia Bolton bao la kwanza dakika ya 6 baada ya kuunganisha kona lakini Nani akasawazisha kwa bao la juhudi binafsi alipoukokota mpira toka mstari wa kati na kutambuka Mabeki wa Bolton kadhaa kisha kufunga kwenye dakika ya 23.
Bolton tena walipata bao la pili dakika ya 67 kufuatia kaunta ataki baada ya kuunasa mpira baada ya kona ya Manchester United kuokolewa na Martin Petrov akamalizia kwa shuti lililombabatiza Darren Fletcher na kutinga.
Ndipo dakika ya 74 frikiki ya Nani ilipounganishwa na Michael Owen wavuni alieingizwa Kipindi cha Pili na kuwaokoa Man United.
Sare ya leo imewafanya Man United washike nafasi ya pili wakiwa na pointi 12 huku Chelsea wakiwa mbele kwa pointi 3 na nyuma ya Man United ni Arsenal na Man City zenye pointi 11 kila mmoja.
Vikosi vilivyoanza:
Bolton: Jaaskelainen, Steinsson, Knight, Ricketts, Robinson, Lee, Holden, Muamba, Petrov, Elmander, Kevin Davies.
Akiba: Bogdan, Taylor, Mark Davies, Klasnic, Moreno, Blake, Alonso.
Man Utd: Van der Sar, O'Shea, Vidic, Jonathan Evans, Evra, Nani, Fletcher, Scholes, Giggs, Rooney, Berbatov.
Akiba: Kuszczak, Owen, Anderson, Smalling, Park, Rafael Da Silva, Macheda.
Refa: Phil Dowd
LIGI ZA ULAYA:

Matokeo Mechi za Jumamosi, Septemba 25
Calcio League A
AC Milan 1 Genoa 0
AS Roma 1 Inter Milan 0
La Liga
Sporting Gijon 0 Valencia 2
Levante 0 Real Madrid 0
Athletic de Bilbao 1 FC Barcelona 3
Bundesliga
VfB Stuttgart 1 Bayer 04 Leverkusen 4
Schalke 04 2 Borussia Monchengladbach 2
Eintracht Frankfurt 2 FC Nurnberg 0
FC St. Pauli 1 BV Borussia Dortmund 3
Bayern Munich 1 FSV Mainz 2
Werder Bremen 3 Hamburger SV 2
Ufaransa Ligi 1
Nice 1 Stade Rennais FC 2
Montpellier HSC 3 Arles 0
Olympique de Marseille 2 FC Sochaux 1
Lorient 2 AS Monaco 1
Caen 0 FC Girondins de Bordeaux 0
Auxerre 2 AS Nancy Lorraine 2
Olympique Lyonnais 0 St.Etienne 1

No comments:

Powered By Blogger