Friday 1 October 2010

Rooney yuko fiti
Straika wa Manchester United Wayne Rooney yuko fiti kuichezea England kwenye mechi ya Makundi ya EURO 2012 na Montenegro hapo Oktoba 12 baada ya kupona enka yake lakini Meneja wake Sir Alex Ferguson amesema ni mapema mno kumchezesha hapo kesho na Sunderland kwenye Ligi Kuu.
Ferguson amesema Rooney alianza mazoezi Alhamisi na mwenyewe yuko tayari kucheza Jumamosi lakini itabidi afikirie sana kwa vile hata kumharakisha.
Kupona kwa Rooney kutamsaidia sana Meneja wa England Fabio Capello kwani Wachezaji wake wengi wa mbele ni majeruhi. Listi ya majeruhi wapo Frank Lampard, Theo Walcott, Jermain Defoe na Bobby Zamora.

No comments:

Powered By Blogger