Wednesday 29 September 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Rubin Kazan 1 Barca 1
Katika mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI iliyoanza mapema leo kupita zote huko Urusi, FC Rubin Kazan walitoka sare na Magwiji wa Ulaya FC Barcelona kwa bao 1-1.
Ni Rubin Kazan ndio walitangulia kupata bao dakika ya 30 kwa penati iliyofungwa na Cristian Noboa na Barca kusawazisha kwa penati dakika ya 60 mfungaji akiwa ni David Villa.
Katika mechi ya leo, Staa Lionel Messi ambae alikuwa majeruhi hivi karibuni, alianzia benchi na kuingizwa kipindi cha pili.

No comments:

Powered By Blogger