Wednesday 29 September 2010

Wenger amfurahia Fabianski
Arsène Wenger amemtaka Kipa wake nambari mbili Lukasz Fabianski kutumia nafasi ya kuumia kwa Manuel Almunia ili adhihirishe yeye ni Kipa bora na anastahili kupewa namba.
Jana Fabianski ndie alikuwa langoni katika ushindi wa ugenini wa 3-1 dhidi ya Partizan Belgrade na aling’ara na pia kuukoa penati.
Mtihani mkubwa kwa Fabianski ni Jumapili ijayo wakati Arsenal watakapotua Stamford Bridge kucheza na Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu Chelsea ambao pia ni vinara wa Ligi.
Wenger alitamka: “ Fabianski alicheza vizuri. Tumemwona Mchezaji yuleyule tunaemwona mazoezini. Nina hakika atakuwa Kipa bora, anataka uzoefu tu!"
EUROPA LIGI: Kesho ni lundo la mechi!
• FC Utrecht v Liverpool: Gerrard apumzishwa!
• Man City v Juventus
Kesho Liverpool watakuwa huko Uholanzi kucheza mechi yao ya pili ya Kundi lao la EUROPA LIGI watakapokutana na FC Utrecht lakini Nahodha wao Steven Gerrard hatasafiri nao baada ya Meneja Roy Hodgson kuamua kumpumzisha.
Pia Mlinzi Daniel Agger ameachwa katika Kikosi hicho lakini Staa Fernando Torres yumo katika Kikosi cha Wachezaji 20 waliosafiri.
Mmoja wa Wachezaji ambae yumo Kikosini ni Dirk Kuyt ambae ni Mchezaji wa zamani wa FC Utrecht.
Hapo Septemba 16, Liverpool iliifunga Steaua Bucharest 4-1 katika mechi yao ya kwanza ya Kundi lao.
Kikosi kamili kilichosafiri:
Reina, Jones, Johnson, Kelly, Kyrgiakos, Skrtel, Carragher, Shelvey, Poulsen, Lucas, Rodriguez, Spearing, Babel, Meireles, Jovanovic, Cole, Kuyt, Eccleston, Ngog, Torres.
Nao Manchester City, baada ya ushindi wa 2-0 ugenini huko Austria walipowachapa Red Bull Salzburg, kesho watakuwa nyumbani kuwakwaa Wakongwe wa Italia Juventus ambao walitoka sare 3-3 na ‘vibonde’ Lech Poznan kutoka Poland katika mechi yao ya kwanza ya Kundi hili.
RATIBA YA MECHI:
Alhamisi, 30 Septemba 2010
Borussia Dortmund v Sevilla
CSKA Moscow v Sparta Prague
CSKA Sofia v FC Porto
FC Metalist Kharkiv v PSV Eindhoven
FC UTRECHT V LIVERPOOL
Hajduk Split v Anderlecht
Odense BK v VfB Stuttgart
Paris SG v Karpaty Lviv
Rapid Vienna v Besiktas
Sampdoria v Debrecen
Steaua Bucharest v Napoli
Young Boys v Getafe
Zenit St Petersburg v AEK Athens
AA Gent v Lille
Atletico Madrid v Bayer Leverkusen
BATE Borisov v AZ Alkmaar
FC Sheriff Tiraspol v Dynamo Kiev
Lech Poznan v Red Bull Salzburg
MAN CITY V JUVENTUS
PAOK Salonika v Dinamo Zagreb
Palermo v Lausanne Sports
Rosenborg v Aris Salonika
Sporting v Levski Sofia
Villarreal v Club Bruges

No comments:

Powered By Blogger