Monday 24 November 2008

FIFA CLUB WORLD CUP JAPAN 2008 & FIFA CONFEDERATIONS CUP SOUTH AFRICA 2009:

Wadau wengi wa Soka wanasubiri kwa hamu mashindano makubwa ya kandanda yanayoandaliwa na FIFA ambayo yanakuja hivi karibuni.
Mwezi ujao, Desemba 2008, huko Japan, Klabu Bingwa za Mabara mbalimbali hapa duniani watajimwaga kuwania Ubingwa wa Klabu Duniani ambao rasmi unaitwa FIFA Club World Cup Japan 2008. Mashindano haya yatafunguliwa rasmi Desemba 11 huko Uwanja wa Taifa mjini Tokyo, Japan na Fainali itachezwa Uwanja wa Kimataifa wa Yokohama mjini Yokohama, Japan tarehe 21 Desemba 2008.
Mwakani, mwezi Juni, huko Afrika Kusini, ambao ndio wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010, watakuwa wenyeji wa Kombe la Mabara ambalo rasmi hujulikana kama FIFA Confederations Cup South Africa 2009 ambalo hushindaniwa na Timu za Taifa ambazo ni Bingwa wa Mabara. Kawaida Kombe hili huchezwa kwa mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia zinazofuatia ikiwa kama ni fungua pazia na vilevile kutesti maandalizi ya Fainali za Kombe la Dunia.

Kwenye FIFA Club World Cup Japan 2008, Klabu zitakazocheza ni:

-Klabu Bingwa ya Asia: Gamba Osaka kutoka Japan

-Klabu Bingwa ya Afrika: Al Ahly ya Misri

-Klabu Bingwa ya Marekani ya Kati: Pachuca toka Mexico

-Klabu Bingwa ya Marekani ya Kusini: Liga de Quito toka Ecuador

-Klabu Bingwa ya Nchi za Baharini: Waitakere United toka New Zealand

-Klabu Bingwa ya Ulaya: Manchester United toka Uingereza

-Mshindi wa Pili wa Klabu Bingwa ya Asia: Adelaide United toka Australia [Timu hii imeingizwa kwa sababu Klabu Bingwa ya Asia inatoka Japan ambao ndio wenyeji wa mashindano].

Kwenye FIFA Confederations Cup South Africa 2009, nchi zitakazoshiriki zimegawanywa makundi mawili kama ifuatavyo:

KUNDI A

-South Africa [Mwenyeji]

-Iraq [Bingwa wa Asia]

-New Zealand [Bingwa wa Nchi za Bahari]

-Spain [Bingwa wa Ulaya]

KUNDI B

-USA [Bingwa wa Marekani ya Kaskazini]

-Italy [Bingwa wa Dunia]

-Brazil [Bingwa wa Marekani ya Kusini]

-Egypt [Bingwa wa Afrika]

RATIBA YA FIFA CLUB WORLD CUP JAPAN 2008:

-11 Desemba 2008: MECHI YA 1: Adelaide United v Waitakere United

-13 Desemba 2008: MECHI YA 2: Al Ahly v Pachuca

-14 Desemba 2008: MECHI YA 3: MSHINDI MECHI YA 1 v Gamba Osaka

-17 Desemba 2008: MECHI YA 4: MSHINDI MECHI YA 2 v Liga de Quito

-18 Desemba 2008:
MECHI YA 5: MSHINDI MECHI YA 3 v Manchester United

-21 Desemba 2008: FAINALI: MSHINDI MECHI YA 4 v MSHINDI MECHI YA 5

RATIBA YA FIFA CONFEDERATIONS CUP SOUTH AFRICA 2009:

-14 Juni 2009: KUNDI A: South Africa v Iraq

-14 Juni 2009: KUNDI B: Brazil v Egypt
[RATIBA KAMILI TUTAITOA BAADAE]

No comments:

Powered By Blogger