Tuesday 25 November 2008


UEFA CHAMPIONS LEAGUE:


Villareal v Manchester United

Mabingwa watetezi Man U leo usiku wanashuka uwanjani Estadio El Madrigal kupambana na wenyeji wao Villareal katika mechi ya KUNDI E ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Kipa nambari wani wa Mabingwa hao, Edwin Van der Sar, ameachwa kwa kile Meneja Sir Alex Ferguson amekiita kumpumzisha na kutoa nafasi kwa Makipa wengine yaani Ben Foster au Kuszczak.
Man U na Villareal, ambao wote wana pointi 8, wanahitaji pointi moja tu ili kusonga mbele.
Leo Man U watakutana na Mchezaji wao wa zamani Mtaliana Giuseppe Rossi ambae kwa sasa ni Mshambuliaji wa kutumainiwa wa Villareal.
Mechi nyingine katika Kundi hili ambayo pia inachezwa leo ni kati ya Aalborg na Celtic. Timu hizi zina pointi 2 kila moja.
Kikosi cha Man U kilichosafiri kwenda huko Madrid, Spain ni:
Foster, Kuszczak, Rafael, O'Shea, Ferdinand, Vidic, Evans, Evra, Ronaldo, Park, Anderson, Fletcher, Carrick, Giggs, Nani, Rooney, Tevez, Possebon, Gibson, Manucho.

Arsenal v Dynamo Kiev

Baada ya vipigo viwili mfululizo kwenye LIGI KUU UINGEREZA vya mabao 2-0 na Aston Villa na 3-0 na Man City, leo Arsenal wanaingia uwanjani kwao Emirates Stadium huku wakiwa na Kepteni mpya, Cesc Fabregas, kupambana na Dynamo Kiev katika mechi ya KUNDI G ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Mechi nyingine katika Kundi hili inayochezwa leo ni kati ya Fenebahce v FC Porto.
Mpaka sasa katika Kundi hili, Arsenal anaongoza akiwa na pointi 8 akifuata FC Porto pointi 6, Dynamo Kiev pointi 5 na Fenerbahce pointi 2.
Timu ya Arsenal itatokana na Wachezaji:
Almunia, Hoyte, Gallas, Silvestre, Clichy, Ramsey, Fabregas, Denilson, Vela, Van Persie, Bendtner, Fabianski, Song, Djourou, Wilshere, Gibbs, Lansbury, Simpson.

No comments:

Powered By Blogger