Friday 28 November 2008

UEFA CUP:

NEC NIJMEGEN 0 TOTTENHAM 1

Bao lililofungwa na Jamie O'Hara dakika ya 14 limewapa ushindi wa bao 1-0 Tottenham wakicheza ugenini Uholanzi dhidi ya NEC Nijmegen.
Bao hilo lilipatikana baada ya Mshambuliaji chipukizi Frazier Campbell ambae yuko Tottenham kwa mkopo akitokea Manchester United kuunganisha krosi ya Gareth Bale iliyogonga mwamba na kumaliziwa na O'Hara.

SCHALKE 04 0 MAN CITY 2

Magoli yaliyofungwa na Benjani Mwaruwaru, raia wa Zimbabwe, na Steven Ireland yamewapa ushindi wa mabao 2-0 Manchester City waliocheza ugenini na Schalke 04 ya Ujerumani.

No comments:

Powered By Blogger