Tuesday 25 November 2008

Wigan wajinasua toka chini!

Wigan, wakicheza kwao JJB Stadium, wameipachika Everton 1-0 kupitia bao lilofungwa na Henri Camara na kujikwamua kutoka nn'gwe ya kushuka daraja na kuchupa hadi nafasi ya 15.
Camara, anaetoka Senegal, aliingizwa dakika ya 46 kumbadilisha Kapo, alifunga kwenye dakika ya 51 kufuatia pasi ya Luis Antonio Valencia.
Meneja wa Wigan, Steve Bruce [pichani], aliekuwa sentahafu wa Man U wakati Sir Alex Ferguson ni Meneja wa Man U, alizungumza baada ya mechi: 'Mara nyingine soka ni mchezo wa ajabu! Tumecheza vibaya na tumeshinda!'

Timu zilikuwa:

Wigan: Kirkland, Taylor, Bramble, Scharner, Figueroa, Valencia, Brown, Palacios, Cattermole, Kapo (Camara 46), Heskey.
Akiba [hawakucheza]:Pollitt, Kilbane, Koumas, De Ridder, Cywka, Routledge.
Goli: Camara 51.

Everton: Howard, Neville (Baines 85), Yobo, Jagielka, Lescott, Cahill, Fellaini, Arteta, Osman, Saha (Anichebe 65), Yakubu.
Akiba [hawakucheza]: Nash, Castillo, Rodwell, Jutkiewicz, Gosling.
Watazamaji: 18,344
Refa: Rob Styles

No comments:

Powered By Blogger