Thursday 21 January 2010

Arsenal watwaa uongozi wa Ligi Kuu
• Refa azua mzozo!!
Jana Arsenal walikwea kilele cha Ligi Kuu baada ya kuipiga Bolton mabao 4-2 huko Uwanja wa Emirates lakini ilibidi watoke nyuma baada ya kupigwa bao 2-0 katika 28 za kwanza za mchezo.
Bolton walifunga kupitia Gary Cahill na Matthew Taylor kwa penalti.
Arsenal walipata mabao yao kupitia Tomas Rosicky na Cesc Fabregas aliesawazisha kisha Thomas Vermaelen akafunga bao la 3 na Andrey Arshavin akaweka la nne.
Lakini mechi hii ilizua utata mkubwa kwa goli la pili la Arsenal la kusawazisha ambalo lilianza kwa Beki wa Arsenal Gallas kumchezea rafu mbaya na kumuumiza Mark Davies lakini Refa Alan Wiley hakupiga filimbi ya rafu wala kusimamisha mpira na Arsenal wakaenda mbele na kufunga bao lao la pili la kusawazisha.
Meneja wa Bolton Owen Coyle ameiita rafu ya Gallas si rafu bali ni ‘shambulizi!’
Kwa ushindi huo sasa Arsenal wamefungana pointi na Chelsea wote wakiwa na pointi 48 lakini Arsenal yuko mbele kwa tofauti ya magoli.
Hata hivyo Chelsea wamecheza mechi moja pungufu.
Nyuma yao kwa pointi moja yuko Manchester United.
VIKOSI Vilivyoanza:
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Clichy, Fabregas, Denilson, Diaby, Rosicky, Arshavin, Eduardo.
Akiba: Fabianski, Vela, Walcott, Silvestre, Traore, Eastmond, Emmanuel-Thomas.
Bolton: Jaaskelainen, Steinsson, Cahill, Knight, Robinson, Lee, Mark Davies, Muamba, Cohen, Taylor, Kevin Davies.
Akiba: Al Habsi, Samuel, Elmander, Klasnic, Ricketts, McCann, Andrew O'Brien.
Refa: Alan Wiley
Carling Cup: Villa ipo Fainali Wembley!!
• Villa 6 Blackburn 4!!
• Refa pia azua mgogoro!!!
Katika mechi ya pili ya marudiano ya Nusu Fainali ya Kombe la Carling iliyochezwa jana Park, Aston Villa wameweza tena kuifunga Blackburn safari hii ikiwa ni mabao 6-4 na hivyo kuingia Fainali itakayochezwa Wembley Februari 28 na watakutana na mshindi wa mechi kati ya Manchester United na Manchester City.
Katika mechi ya kwanza, Villa waliishinda Blackburn bao 1-0 huko Ewood Park.
Jana Blackburn walikuwa mbele kwa bao 2-0 ndani ya dakika 26 za kwanza kwa mabao yaliyofungwa na Klasnic lakini Villa wakasawazisha kupitia Warnock na Milner huku bao moja likiwa la utata mkubwa.
Kisha Beki wa kutumainiwa wa Blackburn, Chris Samba, akapewa Kadi Nyekundu na kipindi cha pili Villa wakaongeza mabao kupitia Agbonlahor, Heskey, Young na moja Nzonzi wa Blackburn alijifunga mwenyewe.
Meneja wa Blackburn, Sam Alladyce, amemponda Refa Atkinson kwa kuchangia Timu yake kufungwa.
Alladyce amedai Refa huyo alifumbia macho rafu ya Agbonlahor kwa Ryan Nelsen iliyomfanya Warnock apate mwanya kufunga na pia kumpa Kadi Nyekundu Samba kulikuwa ni uamuzi mkali kupindukia.
Kuyt aipa ushindi Liverpool!!
Mabao mawili yaliyofungwa na Mshambuliaji wa Liverpool ambae siku zote anajituma kupindukia, Dirk Kuyt, yameleta ahueni huko Anfield baada ya kuandamwa na mikosi ya kufungwa na matokeo mabaya kwa Liverpool na hata watu kuanza kumsakama Meneja wa Liverpool Rafa Benitez.
Kuyt aliipa ushindi Liverpool dhidi ya Tottenham katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa jana usiku huko Anfield.

No comments:

Powered By Blogger