Sunday 17 January 2010

Kwingineko ULAYA:
-Italia: Ronaldinho awasha 3 mguuni kwake! Juve yawashwa!! Inter sare!!
-Spain: Barca kidedea, Real kilio!!!
Ronaldinho alifunga bao 3 mguuni kwake na kuiwezesha AC Milan kuinyuka Sienna bao 4-0 leo kwenye mechi ya Serie A huko Italia na hivyo kufanya pengo na Vinara wa Ligi Inter Milan kuwa pointi 6 baada ya Inter Milan kutoka sare 2-2 na Bari hapo jana.
Inter Milan na AC Milan zitapambana kwenye dabi ya Milan wikiendi ijayo.
Nayo Juventus ilifungwa 1-0 na Chievo.
Huko Spain, Mabingwa Barcelona sasa wako pointi 5 mbele ya Real Madrid kwenye La Liga baada ya kuifumua Sevilla 4-0, bao 2 zikipigwa na Lionel Messi.
Na Mahasimu wa Barca, Real Madrid walilizwa ugenini waliponyukwa kibao kimoja na Athletic Bilbao.

No comments:

Powered By Blogger