• Angola v Algeria na Mali v Malawi
• Nani kusonga Robo Fainali?????

Ili wasonge mbele ni lazima Mali waifunge Malawi lakini hilo pia litategemea matokeo mechi ya Angola na Algeria.
Malawi akimfunga Mali basi moja kwa moja atasonga mbele.
Algeria nao wanahitaji wasifungwe ili wawe na matumaini ya kusonga lakini ushindi ndio utawapa uhakika zaidi.
Wenyeji Angola wanahitaji suluhu tu ili kusonga mbele.
JANA:
• Cameroon 3 Zambia 2
• Gabon 0 Tunisia 0
Cameroun jana wajipa uhai wa kusonga mbele Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuichapa Zambia 3-2 katika mechi ya Kundi D huku Gabon wakizidi kujichimbia kwenye uongozi wa Kundi hili baada ya kutoka sare 0-0 na Tunisia katika mechi zilizochezwa jana.
Kwa matokeo hayo, Gabon wako juu wakiwa na pointi 4, Cameroun ana 3, Tunisia 2 na Zambia 1.
Mechi za mwisho za Kundi hili ni Januari 21 na itakuwa Cameroun v Tunisia na Zambia v Gabon huku Timu zote hizo 4 zina matumaini ya kusonga mbele.
LIGI KUU: Arsenal waipiga Bolton, Wenger ajisifia!!
Baada ya kuichapa Bolton bao 2-0 hapo jana kwenye mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa nyumbani kwa Bolton, Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ametamba kuwa sasa Timu yake inaanza kukomaa na wana uwezo wa kutwaa Ubingwa.
Ushindi huo umeifanya Arsenal sasa iwe pointi 3 nyuma ya Vinara Chelsea na pointi 2 nyuma ya Manchester United huku wakiwa na mechi moja mkononi ambayo wataicheza Jumatano hii kwao Emirates kwa kucheza tena na Bolton.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Nahodha Cesc Fabregas katika kipindi cha kwanza na la pili na Fran Merida kipindi cha pili.
No comments:
Post a Comment