Monday 18 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Leo kimbembe cha mechi za mwisho Kundi A!!!
• Angola v Algeria na Mali v Malawi
• Nani kusonga Robo Fainali?????
Mechi zote hizi za Kundi A zitachezwa leo kwa pamoja kuanzia saa 1 usiku saa za bongo kwa ile ya Angola v Algeria kuchezwa Uwanja wa Novemba 11 Luanda na Mali v Malawi kuchezwa Uwanja wa Chimandela huko Cabinda.
Angola wanaongoza Kundi hili wakiwa na pointi 4, Malawi na Algeria wana 3 na Mali wana pointi moja tu.
Ili wasonge mbele ni lazima Mali waifunge Malawi lakini hilo pia litategemea matokeo mechi ya Angola na Algeria.
Malawi akimfunga Mali basi moja kwa moja atasonga mbele.
Algeria nao wanahitaji wasifungwe ili wawe na matumaini ya kusonga lakini ushindi ndio utawapa uhakika zaidi.
Wenyeji Angola wanahitaji suluhu tu ili kusonga mbele.
JANA:
• Cameroon 3 Zambia 2
• Gabon 0 Tunisia 0
Cameroun jana wajipa uhai wa kusonga mbele Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuichapa Zambia 3-2 katika mechi ya Kundi D huku Gabon wakizidi kujichimbia kwenye uongozi wa Kundi hili baada ya kutoka sare 0-0 na Tunisia katika mechi zilizochezwa jana.
Kwa matokeo hayo, Gabon wako juu wakiwa na pointi 4, Cameroun ana 3, Tunisia 2 na Zambia 1.
Mechi za mwisho za Kundi hili ni Januari 21 na itakuwa Cameroun v Tunisia na Zambia v Gabon huku Timu zote hizo 4 zina matumaini ya kusonga mbele.
LIGI KUU: Arsenal waipiga Bolton, Wenger ajisifia!!
Baada ya kuichapa Bolton bao 2-0 hapo jana kwenye mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa nyumbani kwa Bolton, Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ametamba kuwa sasa Timu yake inaanza kukomaa na wana uwezo wa kutwaa Ubingwa.
Ushindi huo umeifanya Arsenal sasa iwe pointi 3 nyuma ya Vinara Chelsea na pointi 2 nyuma ya Manchester United huku wakiwa na mechi moja mkononi ambayo wataicheza Jumatano hii kwao Emirates kwa kucheza tena na Bolton.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Nahodha Cesc Fabregas katika kipindi cha kwanza na la pili na Fran Merida kipindi cha pili.

No comments:

Powered By Blogger