Saturday 23 January 2010

Rooney aipaisha Man U kileleni!!
• Apachika bao 4!!!
Wayne Rooney leo ameiwezesha Manchester United ikae kileleni mwa LigI Kuu England alipofunga bao zote 4 katika ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Hull City kwenye mechi pekee ya Ligi iliyochezwa Old Trafford.
Kwa ushindi wa leo, Man United wana pointi 50 kwa mechi 23, Arsenal pointi 48 kwa mechi 22 na Chelsea pointi 48 kwa mechi 21.
Arsenal na Chelsea zote hazitacheza mechi za Ligi wikiendi hii kwa vile wana mechi za Kombe la FA.
Baadhi ya Washabiki wa Manchester United waliohudhuria mechi hiyo walivaa na kupepea skafu za rangi ya kijani na njano ikiwa ishara ya kuwapinga Wamiliki wa Man U Familia ya Glazer kwa kuiingiza Klabu hiyo kwenye madeni na kutosajili Wachezaji wapya.
Rangi hizo za njano na kijana zilikuwa ndizo rangi za Timu ya Newton Heath iliyoanzishwa mwaka 1878 na baadae kubadilishwa jina kuitwa Manchester United.
Bila shaka Mashabiki hao na wengine wote watakuwa wamepozwa roho baada ya kumuona Beki wao stadi Rio Ferdinand akicheza kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miezi mitatu baada ya kupona maumivu yake na uchezaji wake ulimfurahisha kila mtu.
Hadi mapumziko, Man United walikuwa mbele kwa bao la kwanza la Rooney aliemalizia baada ya mkwaju wa Paul Scholes kutemwa na Kipa Myhill.
Rooney alipachika bao nyingine 3 dakika za 82, 86 na 90.
Vikosi:
Man United: Van der Sar, Rafael, Ferdinand, Evans, Evra [Fabio, 87], Park, Nani, Scholes [Gibson, 72], Fletcher, Owen [Berbatov, 72], Rooney.
Hull City: Myhill, Dawson, Gardner, McShane, Zayatte, Barmby [Mendy, 57], Geovanni [Kilbane, 74], Hunt, Boateng, Fagan, Garcia [Ghillas, 70].
Refa: Steve Bennett

No comments:

Powered By Blogger