Saturday 23 January 2010

Kesho dabi ya Milan: Inter Milan v AC Milan
Inter Milan na AC Milan kesho saa 4 dakika 45 usiku saa za bongo zitaingia Uwanja uitwao Stadio Giuseppe Meazza, nyumbani kwa Inter, katika pambano la Timu za Mji mmoja la Serie A huku Timu zote hizo zikiwa zinafukuzana kileleni mwa Ligi hiyo ya Serie A.
Inter Milan ndie nambari wani akiwa na pointi 46 kwa mechi 20 na AC Milan ni wa pili akiwa na pointi 40 kwa mechi 19.
Katika mechi ya awali mwanzoni mwa Ligi, Inter iliinyuka AC Milan mabao 4-0 lakini hivi karibuni Inter ikiwa chini ya Meneja machachari Jose Mourinho imekuwa ikiyumba mno na katika mechi zake mbili za mwisho dhidi ya Timu dhaifu Bari na Siena iliponea chupuchupu kufungwa na kuambulia sare.
AC Milan, chini ya Meneja Leonardo, na Ronaldinho aliefufuka tena na Washambuliaji wao hatari , Marco Borriello na Alexandre Pato wakisaidiwa na David Beckham, wamekuwa wakipata mafanikio makubwa hivi karibuni kwa Soka lao zuri.
FA Cup: Ferguson Mtoto kuivaa Chelsea!!

Darren Ferguson, miaka 37, ni Meneja wa Klabu ndogo sana iliyo Daraja la Championship ambalo liko chini ya Ligi Kuu iitwayo Preston North End na pia ni Mtoto wa Meneja maarufu na mwenye mafanikio makubwa kwenye historia ya Uingereza, Sir Alex Ferguson wa Manchester United.
Darren Ferguson leo ataiongoza Preston North End Uwanjani kwao Deepdale kucheza na Vigogo Chelsea kwenye Raundi ya 4 ya Kombe la FA.
Baada ya Chelsea kuifumua Sunderland mabao 7-2 hivi juzi, wengi hawawapi Preston nafasi hata chembe.
Lakini Darren Ferguson anasema: “Reading walikwenda Liverpool wakashinda! Leeds walikuwa Old Trafford wakaifunga Man United! Chelsea hawawezi kuwa wanacheza vizuri kila siku!”
Darren Ferguson alianza kazi ya Umeneja Misimu mitatu iliyopita akiwa na Peterborough Timu aliyoipandisha Madaraja mawili mfululizo hadi kuifikisha Championship Msimu huu na akajiuzulu toka Timu hiyo mwezi Novemba mwaka jana.
Amejiunga na Preston mwanzoni mwa Januari.
Kuhusu Baba yake, Darren Ferguson amekiri anaongea nae kila siku na humpa ushauri lakini amesisitiza yeye hutoa maamuzi peke yake.

No comments:

Powered By Blogger