Wednesday 20 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Nigeria yaungana na Misri Robo Fainali!!
Leo Nigeria wameinyuka Msumbiji mabao 3-0 na kuungana na Misri kutoka Kundi C kuingia Robo Fainali.
Mabao ya Nigeria yalifungwa na Osaze Odemwingie, bao 2, na Obafemi Martins, bao moja.
Misri ndio Washindi wa Kundi hili na Nigeria wamechukua nafasi ya pili.
Nao, Misri, katika mechi yao ya kukamilisha ratiba tu, waliipiga Benin 2-0 kwa mabao yaliyofungwa na Al Muhammad na Emad Moteab.
Robo Fainali zitachezwa Jumapili na Jumatatu ijayo.
Kesho ni Kundi D linacheza mechi zake za mwisho na Gabon ndio wanaongoza Kundi hilo wakiwa na pointi 4, Cameroun pointi 3, Tunisia 2 na Zambia moja tu.
Ili kuingia Robo Fainali, Gabon na Cameroun wanahitaji suluhu tu wakati Tunisia na Zambia ni lazima washinde.
MECHI ZA KESHO Januari 21:
[KUNDI D]
Gabon v Zambia
Cameroun v Tunisia
ROBO FAINALI:
Jumapili Januari 24:
Angola v Ghana
Ivory Coast v Algeria
Jumatatu Januari 25:
Misri v Mshindi wa 2 Kundi D
Mshindi wa 1 Kundi D v Nigeria

No comments:

Powered By Blogger