Friday 22 January 2010

Van Nistelrooy kutua West Ham?
Inasemekana West Ham imetoa ofa ya Mshahara wa Pauni Laki 1 kwa wiki ili Straika wa Real Madrid Ruud van Nistelrooy ajiunge kwa mkopo na Klabu hiyo ya Jijini London.
Taarifa hizo zimeenezwa na mmoja wa Wamiliki wapya wa West Ham David Sullivan ingawa hakumtaja kwa jina Straika huyo lakini wadau wanahisi ni Van Nistelrooy ambae kwa sasa hana namba ya kudumu huko Real.
Fergie anataka ushindi kesho ili aukwae uongozi Ligi Kuu
Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United, anahisi sasa Ligi inaingia hatua muhimu na ushindi kwa Timu yake inayocheza na Hull City huko Old Trafford kwenye mechi pekee ya Ligi Kuu hapo kesho ni muhimu sana kwa vile utawafanya waongoze Ligi kwa pointi 2 mbele ya Arsenal na Chelsea wanaofungana kwa pointi kileleni mwa Ligi hiyo.
Ferguson amesema: “Ukishinda mechi zako, uko kileleni! Ni nafasi nzuri kuwepo! Itazame Arsenal, wameshinda mechi zao za hivi karibuni, sasa wako juu wakati watu wengi waliwafuta kwenye Ligi!”
Ferguson pia aliongeza kuwa ushindi kwao ni muhimu hasa kwa vile wikiendi inayofuata watakuwa Emirates kupambana na Arsenal na amesema: “Ni nafasi nzuri kwetu kesho kwani Jumapili ijayo tuko na Arsenal na hiyo ni mechi kubwa! Kisha wiki inayofuata Arsenal wanacheza na Chelsea!! Hizi ni nyakati zinazovutia!!”
Ferdinand kesho ndani ya Old Trafford!!
Hajacheza Miezi mitatu sasa lakini kesho Beki mahiri wa Manchester United na England, Rio Ferdinand, atashuka na Klabu yake kupambana na Hull City kwenye mechi ya Ligi Kuu kama ilivyothibitishwa na Meneja wake Sir Alex Ferguson.
Ferguson ametamka: “Rio amekuwa akifanya vizuri mazoezini. Atacheza Jumamosi.”
Ferdinand amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya mgongo yaliyokuwa pia yakiathiri misuli za miguu na ilibidi apelekwe Jijini London kwa Speshelisti.
Ferguson vile vile amesema Majeruhi mwingine wa muda mrefu, Owen Hargreaves, kwa sasa yupo kwenye mazoezi makali na Kikosi cha Akiba na jina lake litakuwemo kwenye Listi ya Wachezaji 25 wanaotakiwa kusajiliwa UEFA kwa ajili ya Mashindano ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE ambako Man U watacheza na AC Milan kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 mwezi Februari.

No comments:

Powered By Blogger