Saturday 23 January 2010

Steve Bruce aishambulia Liverpool!!!
Bosi wa Sunderland Steve Bruce ameishambulia vikali Liverpool kwa kumrubuni Straika wao Kenwyne Jones na kutangaza kuwa watamchukua kwa mkopo.
Bruce ameziita habari hizo ni utovu wa nidhamu na zina lengo za kumchanganya Mchezaji wao ili apate matumaini mabovu.
Bruce amesema: “Wao hawajoangea na mtu yeyote wa Klabu hii kuhusu Jones. Wanatangaza kwa umma kumchukua yeye na bila shaka washaongea nae kinyemela! Hivi watafikiriaje sisi tukisema tunamchukua Steven Gerrard kwa mkopo?”
Neville & Tevez waonywa na FA
Nahodha wa Manchester United Gary Neville na Mchezaji wa Manchester City Carlos Tevez wametakiwa wajitahadharishe ili wasichukuliwe hatua na kuadhibiwa kufuatia msuguano kati yao uliotokea kwenye mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Carling Cup wiki iliyopita huko City of Manchester Stadium ambako Man City waliifunga Man United 2-1 Mfungaji wa bao 2 za City akiwa Tevez.
Kabla ya mechi Neville alikaririwa akisema kuwa Tevez, ambae aliichezea Man United kwa mkopo kabla ya kuhamia City na ilitakiwa ilipwe Pauni Milioni 25 ili awe Mchezaji wa kudumu wa Man U, hakuwa na thamani ya Pauni Milioni 25 na inaelekea hilo lilimkera Tevez na alipofunga mabao yake kwenye mechi kati ya Timu hizo wiki iliyopita alikuwa akienda kushangilia mbele ya benchi la Man U. Ilidaiwa kuwa wakati Tevez anashangilia Neville alionekana akitoa ishara ya kidole kimoja ambayo wengi hutafsiri ni matusi.
Baada ya matukio hayo kwenye mechi hiyo iliripotiwa kuwa Tevez akihojiwa na TV ya kwao Argentina alimwita Neville ni ‘zuzu’ na ‘mlamba viatu’ na ndio maana kila alipofunga goli alikuwa akienda mbele yake kumkejeli.
FA, ikishirikiana na Polisi wa Manchester, wamekuwa wakijaribu kutuliza na kuipoza hali kabla ya marudiano ya Nusu Fainali ya Carling Cup kati ya Vilabu hivyo vya Jijini Manchester Uwanjani Old Trafford Jumatano ijayo.

No comments:

Powered By Blogger