Sunday 17 January 2010

LIGI KUU: Blackburn 2 Fulham 0
Blackburn waliokuwa hawajashinda katika mechi 9 zilizopita za Ligi Kuu leo wakiwa nyumbani Ewood Park wameifunga Fulham Timu inayofanya vizuri kwenye ligi kwa mabao 2-0.
Kona ya Benni McCarthy ilizua kizaazaa langoni mwa Fulham na kumdondokea Beki wa Blackburn Chris Samba aliepiga ndochi na kuandika bao la kwanza katika dakika ya 25.
Kipindi cha pili dakika ya 65 kufuatia frikiki ya Benni McCarthy Beki Ryan Nelsen aliunganisha kichwa na kufunga bao la pili.
Kwa ushindi huo Blackburn wako nafasi ya 12 wakiwa na pointi 24 kwa mechi 22 na Fulham wako nafasi ya 9 kwa mechi 21 na pointi 27.

No comments:

Powered By Blogger