Monday 18 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Angola na Algeria Robo Fainali!!!!
Angola 0 Algeria 0
Wenyeji wa Mashindano Angola na Algeria zilitoka suluhu ya 0-0 iliyowabeba wote wawili kuingia Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika katika mechi iliyochezwa Mji Mkuu wa Angola Luanda Uwanjani Novemba 11 na hivyo kuwabwaga nje Mali na Malawi waliokuwa wakipambana katika mechi nyingine.
Kufuatana na sheria za Mashindano hayo, ingawa Algeria na Mali zilimaliza zikiwa sawa wakiwa na pointi 4 kila mmoja na ingawa Mali alikuwa na goli nyingi, ni Algeria amepita kwa vile tu waliifunga Mali Timu hizo zilipokutana.
Mali 3 Malawi 1
Goli mbili za haraka za Kanoute kwenye sekundi ya 40 ya mchezo na Seydou Keita kwenye dakika ya 4 tu pamoja na la 3 la Mamadou Bagayoko yaliipa ushindi Mali wa mabao 3-1 lakini hilo halikuweza kuwafinikisha kuingia Robo Fainali kwani suluhu ya 0-0 ya Angola na Algeria iliwabeba wawili hao kusonga mbele.
Bao la Malawi lilifungwa na Russell Mwafulirwa.
MECHI ZA KESHO Jumanne Januari 19:
[KUNDI B]
Burkina Faso v Ghana
Ivory Coast v Togo [HAMNA Togo imejitoa]
Henry apona rungu la FIFA
Mshambuliaji wa Ufaransa Thierry Henry hatapewa adhabu yeyote na FIFA kufuatia kitendo chake cha kuucheza mpira kwa mkono kisha kumpasia William Gallas alieisawazishia Ufaransa katika muda wa nyongeza dhidi ya Ireland na kuibeba Nchi hiyo kuingia Fainali za Kombe la Dunia.
Ufaransa ilikuwa imeshinda mechi ya kwanza 1-0.
Baada ya kitendo hicho cha Henry kuliibuka mzozo mkubwa huku kukiwa na mbiu ya mechi kurudiwa lakini FIFA iligomea hatua hiyo na badala yake ikapeleka kesi ya Henry kwenye Kamati ya Nidhamu ambayo leo imeamua kuwa hamna misingi yeyote ya kisheria kufuatana na kanuni za FIFA kumwadhibu Henry.
Kanuni za FIFA hutambua tu na huweza kuchukua adhabu ikiwa mtu anazuia kufungwa goli kwa mkono ikiwa yeye si Kipa lakini ipo kimya endapo mtu anatumia mkono kufunga goli.
Mwenyewe Henry aliomba radhi kwa kitendo chake.

No comments:

Powered By Blogger