Tuesday 19 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Ghana iko Robo Fainali!!!
Bao la dakika ya 30 la Mwana wa Abedi Ayew Pele, aitwae Ayew, limeifikisha Ghana Robo Fainali baada ya kuwatoa Burkina Faso kwa bao hilo moja.
Burkina Faso walikuwa wakitaka sare tu ili wao ndio wasonge mbele.
Sasa Januari 24 ndio zitakuwa Robo Fainali za kwanza kwa Angola kucheza na Ghana huku Ivory Coast kukutana na Algeria.
Robo Fainali nyingine zitachezwa Januari 25 na tayari Misri yuko huko huku ameshajihakikishia kuwa Mshindi wa kwanza wa Kundi C na hivyo atacheza na Mshindi wa Pili wa Kundi D ambalo wapo Cameroun, Gabon, Zambia na Tunisia.
Mechi nyingine ya Robo Fainali ya hiyo Januari 25 ni kati ya Mshindi Kundi D na Mshindi wa Pili Kundi C ambae pengine ni Nigeria, Benin au Zambia.
MECHI ZA KESHO Januari 20:
[saa 1 usiku, bongo taimu]
[KUNDI C]
Egypt v Benin
Nigeria v Mozambique

No comments:

Powered By Blogger