Monday 18 January 2010

HABARI KWA UFUPI:
• Rio kurudi uwanjani Jumatano!!
Beki mahiri wa Manchester United, Rio Ferdinand, ambae hajacheza miezi mitatu sasa inasemekana huenda akaingia dimbani Jumatano wakatika Man U watakapotua City of Manchester Stadium kukwaana na Mahasimu wao Manchester City katika dabi ya mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Carling Cup.
Mechi ya mwisho kwa Rio ilikuwa Oktoba 25 walipofungwa na Liverpool.
• Essien nje Angola!!
Kiungo wa Ghana, Michael Essien, hataweza kucheza tena kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika huko Angola baada ya kuumia goti mazoezini.
Madaktari wamesema Mchezaji huyo itabidi awe nje si chini ya mwezi mmoja.
• Zaki ndani ya Hull City!!!
Straika wa Zamalek ya Misri, Amr Zaki, amesaini kuichezea Timu ya Ligi Kuu England Hull City kwa mkopo hadi mwishoni mwa Msimu.
Zaki aliichezea Wigan kwa mkopo Msimu uliopita lakini hakupata mkataba wa kudumu baada ya kukwaruzana na aliekuwa Meneja wa Wigan wakati huo Steve Bruce.
Zaki ambae pia huchezea Timu ya Taifa ya Misri hayupo Angola na Timu hiyo baada ya kuumia.
• Qatar kuinunua Man U?
Kufuatia ziara yao ya siku 4 huko Doha, Qatar wiki iliyokwisha, kumeibuka stori za Magazeti ya Uingereza kuwa Nchi ya Qatar ambayo ina Utajiri mkubwa hasa wa gesi ipo mbioni kuinunua Klabu ya Manchester United kutoka kwa Wamiliki wake Ukoo wa Kimarekani wa Glazer.
Hata hivyo Mamlaki ya Rasilmali ya Qatar imekataa kuthibitisha habari hizo.

No comments:

Powered By Blogger