Saturday 23 January 2010

Man U wakusanya Pauni Milioni 504 kwa mauzo ya Hati za Dhamana
Manchester United wamefanikiwa kukusanya zaidi ya Pauni Milioni 504 kutokana na mauzo ya Hati za Dhamana na makusanyo hayo yatasaidia ulipaji wa deni la Pauni Milioni 509 linaloikabili Klabu na pia kuwasaidia Wamiliki wa Klabu hiyo Familia ya Glazer kulipia deni lao la Pauni Milioni 202.
Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester United David Gill amekuwa kwenye ziara ya Dunia nzima wiki za hivi karibuni ili kutangaza Hati hizo za Dhamana ambazo zitaendelezwa hadi Februari 2017 na sasa ziara hiyo ya Gill imezaa mafanikio makubwa kwani Hati hizo zimeuzwa kupindukia na kupita matarajio.
Msemaji wa Familia ya Glazer amesema biashara hiyo italeta uwazi hapo Klabuni kwa miaka 7 ijayo na pia kurahisisha uendeshwaji wa Klabu na hivyo kuweza kusajili Wachezaji wapya.

No comments:

Powered By Blogger