
Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester United David Gill amekuwa kwenye ziara ya Dunia nzima wiki za hivi karibuni ili kutangaza Hati hizo za Dhamana ambazo zitaendelezwa hadi Februari 2017 na sasa ziara hiyo ya Gill imezaa mafanikio makubwa kwani Hati hizo zimeuzwa kupindukia na kupita matarajio.
Msemaji wa Familia ya Glazer amesema biashara hiyo italeta uwazi hapo Klabuni kwa miaka 7 ijayo na pia kurahisisha uendeshwaji wa Klabu na hivyo kuweza kusajili Wachezaji wapya.
No comments:
Post a Comment