Friday 22 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Ufafanuzi mechi za Robo Fainali ni Misri v Cameroun na Zambia v Nigeria!!!
Sheria za kujikanganya za CAF jana zilijitokeza na kuwapoteza Wadau wengi wakiwemo Waandishi wa Habari na hata Timu ya Gabon ambao mara baada ya mechi yao waliyofungwa 2-1 na Zambia walishangilia wakijua wao ndio wameingia Robo Fainali kwa vile Cameroun walitoka sare 2-2 na Tunisia lakini wakalizwa walipofafanuliwa wao ni ‘auti’!
Awali ilitangazwa Robo Fainali ni Msiri v Zambia na Nigeria v Cameroun ikimaanisha Kundi D Mshindi wa Kwanza ni Cameroun na Mshindi wa Pili ni Zambia lakini sasa CAF imefafanua kuwa katika Kundi hilo Zambia, Cameroun na Gabon zote zilifungana kwa kuwa na pointi 4 kila mmoja na hivyo kilichoamua nafasi ni hizo sheria za kushangaza za CAF za kuchukua matokeo ya mechi za uso kwa uso za Timu zilizofungana ili kuamua nani mshindi.
Hivyo, Zambia ameibuka kama Mshindi wa 1, Cameroun wa 2 na Gabon wa 3 kwa vile katika mechi za kwa uso kwa uso kati ya Timu hizo 3, Zambia ndie alikuwa na magoli mengi ya kufunga.
Matokeo mechi kati yao:
-Gabon 1 Cameroun 0
-Cameroun 3 Zambia 2
-Zambia 2 Gabon 1
Magoli ya kufunga:
-Zambia 4
-Cameroun 3
-Gabon 2
RATIBA ROBO FAINALI:
Jumapili Januari 24:
Angola v Ghana
Ivory Coast v Algeria
Jumatatu Januari 25:
Misri v Cameroun
Zambia v Nigeria

No comments:

Powered By Blogger