Saturday 30 January 2010

CAF yaifungia Togo!!!
Togo wamefungiwa kutocheza Mashindano mawili yafuatayo ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kujitoa kwenye Fainali za Mashindano hayo yanayofanyika Angola kufuatia basi walilokuwa wakisafiria kushambuliwa kwa risasi na kuuliwa Dereva wake, Kocha Msaidizi na Afisa Habari wa Togo.
Baada ya maafa hayo Serikali ya Togo iliamuru Timu ya Togo irudi nyumbani.
Basi hilo la Togo lilitokea Congo na lilikuwa limeshaingia Angola kwenye Jimbo la Cabinda lenye Waasi na likashambuliwa likiwa njiani kwenda kwenye kituo chao Mji wa Cabinda walikotakiwa kuwa Kundi moja na Ghana, Ivory Coast na Burkina Faso.
Rais wa CAF, Issa Hayatou, amethibitisha kuwa Togo imefungiwa kwa vile Serikali iliingilia masuala ya soka.

No comments:

Powered By Blogger