Tuesday 26 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Nigeria yaitoa Zambia kwa matuta!!
Ni mechi ambayo ni lazima Zambia wataiota kwa muda mrefu sana kwani ushindi ulikuwa mweupe kwao baada ya kuutawala mchezo na kukosa nafasi nyingi sana.
Zambia, wakiwa na Vijana wadogo kiumri kama vile Mbola mwenye miaka 16 tu na wengi wenye maumbo madogo tu, waliwafunika Masupastaa wa Nigeria akina Shittu, Etuhu, Mikel, Odemwingie, Yakubu na Martins.
Licha ya kumiliki mechi yote na pia Nigeria kucheza mtu 10 kipindi cha pili cha nyongeza ya dakika 30 baada ya Apam kutolewa kwa Kadi Nyekundu, Zambia walishindwa kupata goli.
Ndipo ikaja mikwaju mitano ya penalti na Zambia wakakosa moja iliyookolewa na Kipa Enyeama.
Nusu Fainali Nigeria watacheza na Watani wao wa Jadi Ghana.
Vikosi vilivyoanza:
Zambia: Mweene, Musonda, Sunzu, Himonde, Mbola, Chris Katongo, Nyirenda, Njobvu, Felix Katongo, Chamanga, Mulenga
Nigeria: Enyeama, Mohammed, Apam, Shittu, Echiejile, Etuhu, Kaita, Mikel, Odemwingie, Yakubu, Obasi
Nusu Fainali Alhamisi Januari 28
[saa 1 usiku]
Ghana V Nigeria
[saa 4 na nusu usiku]
Algeria V Misri

No comments:

Powered By Blogger