Sunday 24 January 2010

Hamburg wamchota Van Nistelrooy
Mshambuliaji wa Real Madrid Ruud van Nistelrooy amejiunga na Hamburg ya Ujerumani kwa mkataba wa miezi 18-month.
Veterani huyo mwenye umri wa miaka 33 alihusishwa na kuhamia England aidha West Ham au Tottenham lakini Tottenham ikajitoa kumchukua walipoona hawatomudu Mshahara wake wakati Mchezaji mwenyewe aliikataa West Ham.
Van Nistelrooy amekuwa hapati namba Real na kuhama kwake ni kutafuta namba ya kudumu ili apate nafasi ya kuchukuliwa Timu ya Taifa ya Uholanzi kuchezea Kombe la Dunia mwezi Juni huko Afrika Kusini.
KOMBE LA AFRIKA: Robo Fainali zaanza leo!!!
Angola v Ghana
Leo Robo Fainali ya kwanza itakayoanza saa 1 usiku saa za bongo ni ile itakayopigwa Uwanja wa Novemba 11 huko Luanda, Angola na ni kati ya Wenyeji Angola na Ghana.
Angola watafarijika na kupata morali kubwa kwa habari kuwa Flavio ambae ndie Mfungaji Bora wa Mashindano haya mpaka sasa yuko fiti kucheza.
Flavio hakucheza mechi ya mwisho Angola walipokutana na Algeria.
Wakati Ghana walipata shida kutinga Robo Fainali baada ya kupigwa 3-1 na Ivory Coast na kisha kuifunga Burkina Faso 1-0, Wenyeji Angola kwao ilikuwa nafuu kidogo kwani walitoka sare 4-4 na Mali, wakaifunga Malawi 2-0 na kutoka sare 0-0 na Algeria.
Ivory Coast v Algeria
Huko Cabinda, Angola Uwanja wa Taifa wa Chiazi, Ivory Coast na Algeria zitashuka kukwaana katika mechi ya Robo Fainali huku wengi wakiwapa Ivory Coast wenye Mastaa wakubwa kina Drogba na Ndugu wawili Kolo Toure na Yaya nafasi kubwa ya ushindi.
Lakini Algeria si Timu ya mchezo na wengi watakumbuka walivyoiadhiri Misri na kuwabwaga nje ya Kombe la Dunia.
Ivory Coast walikuwa na njia nyepesi kuingia Robo Fainali kwani walicheza mechi mbili tu baada ya Togo kujitoa toka Kundi lao kufuatia maafa waliyopata na katika mechi hizo walitoka droo na Burkina Faso na kisha kuwafunga Ghana 3-1.
Algeria wao walipigwa mechi ya kwanza 3-0 na Malawi, wakafufuka na kuwakung’uta Mali 2-0 na kisha kutoka sare 0-0 na Wenyeji Angola.
Everton wambeba Senderos kwa mkopo
Everton na Arsenal zimekubaliana Mchezaji Philippe Senderos aende Everton kwa mkopo hadi mwishoni mwa Msimu huu.
Mlinzi huyo wa Arsenal kutoka Uswisi mwenye umri wa miaka 24, amekuwa hana namba Arsenal na Everton wamelazimika kumchukua baada ya kupata pengo kufuatia kuhama kwa Beki wao Lucas Neill aliehamia Klabu ya Uturuki Galatasaray.
Senderos alijunga Arsenal mwaka 2003 kutoka Klabu ya Uswisi Servette na ameichezea Arsenal mechi 117 lakini Msimu uliokwisha alipelekwa AC Milan kwa mkopo na tangu arudi hapo Klabuni amekuwa hapewi namba.
Senderos amesema: “Nataka niondoke! Nataka niwe nacheza ili niwe fiti kwa Fainali za Kombe la Dunia!”

No comments:

Powered By Blogger