Sunday 24 January 2010

KOMBE LA AFRIKA: Wenyeji Angola waaga!!
Bao la dakika ya 16 la Asamoah Gyan limewaliza Angola na kuwatoa nje ya Kombe la Mataifa ya Afrika katika mechi ya Robo Fainali iliyofanyika Mjini Luanda, Angola Uwanja wa Novemba 11 mbele ya halaiki ya Waangola waliohuzunika.
Baada ya bao la Gyan, Angola walifanya wimbi kufuatia wimbi la mashambulizi lakini umaliziaji wao ulikuwa dhaifu hasa Mshambuliaji Manucho aliepata nafasi kadhaa za wazi na pia umahiri wa Kipa wa Ghana Kingston ndio uliowaua Angola.
Ghana wameingia Nusiu Fainali na watakutana na Mshindi kati ya Zambia au Nigeria na mechi hiyo ya Nusu Fainali itachezwa Alhamisi tarehe 28 Januari.
Baada ya muda mfupi ujao, Ivory Coast wataingia dimbani kucheza na Algeria kwenye mechi ya pili ya Robo Fainali ya leo.

No comments:

Powered By Blogger