Tuesday 26 January 2010

Kandanda wiki hii:
Jumanne, Januari 26
LIGI KUU
[saa 4 dak 45 usiku]
Portsmouth v West Ham
Tottenham v Fulham
Wolves v Liverpool
[saa 5 usiku]
Bolton v Burnley
Jumatano, Januari 27
Caling Cup
[saa 5 usiku]
Man United v Man City
LIGI KUU
[saa 4 dak 45]
Aston Villa v Arsenal
Chelsea v Birmingham
[saa 5 usiku]
Blackburn v Wigan
Everton v Sunderland
Alhamisi, Januari 28
Kombe la Mataifa ya Afrika-Nusu Fainali
[saa 1 usiku]
Ghana v Nigeria
[saa 4 na nusu usiku]
Algeria v Misri
LIGI KUU
Jumamosi, Januari 30
[saa 12 jioni]
Birmingham v Tottenham
Fulham v Aston Villa
Hull v Wolves
Liverpool v Bolton
West Ham v Blackburn
Wigan v Everton
[saa 2 na nusu usiku]
Burnley v Chelsea
LIGI KUU
Jumapili, Januari 31
[saa 10 na nusu jioni]
Man City v Portsmouth
[saa 1 usiku]
Arsenal v Man United
LIGI KUU
Jumatatu, Februari 1
[saa 5 usiku]
Sunderland v Stoke

LIGI KUU
Jumanne, Februari 2
[saa 4 dak 45]
Hull v Chelsea
LIGI KUU
Jumatano, Februari 3
Fulham v Portsmouth
Shearer: “Rooney anaibeba Man United”
Alan Shearer, Mshambuliaji wa zamani wa England ambae pia alikuwa Meneja wa Newcastle, ametamka kuwa Wayne Rooney ndio anaibeba Manchester United na bila yake Klabu hiyo ingeyumba.
Shearer amesema: “Wasingekuwa walipo kwenye Ligi bila Rooney.”
Rooney ndie anaeongoza kwa kufunga magoli mengi kwenye Ligi Kuu na anazo goli 19.
Hata hivyo Shearer amekiri kuwika kwa Rooney ni manufaa makubwa kwa England hasa kwa sababu Kombe la Dunia lipo karibuni.
Rio ashitakiwa na FA!!
Sentahafu wa Manchester United, Rio Ferdinand, ameshitakiwa na FA kwa kosa la mchezo mbaya na wa fujo baada ya kunaswa na kamera akimpiga Mshambuliaji wa Hull City Craig Fagan katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa Old Trafford Jumamosi iliyopita ambapo Man United waliifunga Hull mabao 4-0.
Kitendo cha Rio hakikuonekana kwa Refa Steve Bennett na badala yake alimpa Kadi ya Njano Fagan muda mfupi baada ya tukio hilo.
Rio Ferdinand alikuwa akicheza mechi yake ya kwanza baada ya miezi mitatu kwa sababu alikuwa kaumia.
Ferdinand amepewa mpaka Jumatano kujibu mashitaka hayo na anaweza kukubali kosa na hivyo kutumikia kifungo cha mechi 3 au kukana na kesi hiyo ikaanza kusikilizwa Alhamisi.
Akikubali kosa hiyo Jumatano atakuwa huru kucheza Mechi ya siku hiyo hiyo usiku ya Nusu Fainali ya Carling Cup dhidi ya Manchester City na adhabu yake ya mechi 3 itaanza Jumapili Man United watakapocheza na Arsenal.

No comments:

Powered By Blogger