Monday 25 January 2010

Dabi ya Milan: Mtu 9 Inter yawabwaga AC Milan!!
Inter Milan wamejivuta hadi pointi 9 mbele ya Mahasimu wao AC Milan baada ya kuwachapa 2-0 hapo jana kwenye mechi ya Serie A.
Inter ilibidi wacheze muda mwingi wa mechi hiyo wakiwa mtu 10 baada ya Wesley Sneijder kutwangwa Kadi Nyekundu na katika dakika 5 za mwisho walibaki mtu 9 baada ya Beki Lucio kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
Mmoja wa watu walioshuhudia mechi hiyo ni Sir Alex Ferguson ambae alikuja kuwacheki wapinzani wao wa mwezi ujao kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE ACMilan.
Inter Milan walipata bao la kwanza kupitia Diego Milito na Goran Pandev akafunga bao la pili.
Ronaldinho aliwakosesha AC Milan bao wakati penalti yake iliyotolewa baada ya Mbrazil mwenzake Beki wa AC Milan Lucio kuunawa na hivyo kulambwa Kadi Nyekundu kuokolewa na Kipa wa Brazil Cesar.
Pengine Ferguson atapata moyo mkubwa kwa kuiona AC Milan butu lakini Chelsea watapata kiwewe kwa kuwaona wapinzani wao wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE Inter Milan wakiwa wakali kama mbwa mwitu!
KOMBE LA AFRIKA: Leo Robo Fainali tena!!
Misri v Cameroun
Huko Benguela, Angola Uwanjani Ombaka, Mabingwa Watetezi Misri watajimwaga kuchuana na Timu ngumu Cameroun katika mechi ya kwanza ya leo ya Robo Fainali.
Mechi hii itaanza saa 1 kamili saa za bongo.
Zambia v Nigeria
Robo Fainali hii ya pili kwa leo itachezwa Uwanja wa Tundavala huko Lubango na itaanza saa 4 na nusu usiku saa za bongo.
Katika mechi ya leo Nigeria itamkosa Nahodha Joseph Yobo na Zambia itawakosa Kiungo Kalaba Rainford na Beki Kampamba Chintu ambao wamesimamishwa kwa kuwa na Kadi.
Algeria yawatoa Masupastaa kina Drogba!!!
• Algeria 3 Ivory Coast 2
Wengi walidhani Ivory Coast wametinga Robo Fainali pale Keita alipoingiza bao dakika ya 89 na kufanya gemu kuwa 2-1 lakini Algeria wakasawazisha dakika ya 90 kupitia Bougherra na ngoma ikaingizwa kwenye muda wa nyongeza wa nusu saa na ndipo Algeria wakaibuka kidedea baada ya Mchezaji wa Klabu ya Blackpool ya England, Bouazza, kupachika bao la 3 na la ushindi dakika ya 93.
Ivory Coast ndio walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 4 Mfungaji akiwa Kalou na Algeria wakarudisha dakika ya 40 kwa bao la Matmour.
Algeria atacheza Nusu fainali na Mshindi wa leo kati ya Misri na Cameroun.
Wenger ajibebesha lawama!!
Arsene Wenger amekubali kuwa lawama zote za kutupwa nje ya Kombe la FA baada ya kuchapwa 3-1 na Stoke City hapo jana ni za kwake yeye baada ya kupanga Kikosi dhaifu.
Wenger amesema alikuwa hana njia ila kupanga Timu ya aina hiyo kwa vile wanakabiliwa na mechi ngumu mfululizo dhidi ya Aston Villa, Manchester United, Chelsea na Liverpool ndani ya siku 14 zijazo wakianzia Jumatano hii.

No comments:

Powered By Blogger