Friday 29 January 2010

Mutu yamkuta tena!!!
• Ni madawa yamtia matatani!!!!
Mshambuliaji wa Fiorentina Adrian Mutu amegundulika kutumia madawa yaliyopigwa marufuku na sasa yuko matatani na CONI, Kamati ya Olimpiki ya Italia, hii ikiwa ni mara ya pili kwa Mutu kukumbana na rungu la utumiaji wa madawa yaliyopigwa marufuku.
Mutu, miaka 31 kutoka Romania, aligundulika na chembechembe za dawa iitwayo ‘sibutramine’ ambayo hutumika kupunguzia unene na ambayo ipo kwenye listi ya dawa marufuku kwa Wanamichezo.
Ugundizo huo ulitokea baada ya mechi ya Serie A kati ya Klabu yake Fiorentina na Bari iliyofanyika Januari 10 na Mutu alipiga bao kwenye mechi hiyo Fiorentina waliyoshinda 2-1.
Mwaka 2004 Mutu aligundulika akitumia kokeni na kufungiwa pamoja na kufukuzwa na Klabu yake ya wakati huo, Chelsea, ambayo ilimshitaki na kumdai Mutu alipe fidia kwa kukiuka mkataba.
Mutu anatakiwa ailipe Chelsea Pauni Milioni 15 na kesi ipo Mahakamani baada ya Mutu kukata rufaa.

No comments:

Powered By Blogger