Thursday 28 January 2010

Rio kifungo mechi 4!!!!!!!!!

Rio Ferdinand amefungiwa mechi 4 baada ya rufaa yake ya kupinga shitaka la kushambulia kutupwa na Jopo Huru la Nidhamu.
Rio alishitakiwa kwa kumpiga Straika wa Hull City Craig Fagan katika mechi ya Ligi Kuu ya Jumamosi iliyopita na tukio hilo halikuonwa na Refa Steve Bennett.
Kawaida kosa kama hilo Mchezaji hufungiwa mechi 3 tu lakini ukikata rufaa na kushindwa hiyo rufaa ni kawaida pia kuongezewa kifungo cha mechi moja na hilo ndilo lililomkuta Rio Ferdinand.
Kwa hiyo Rio atazikosa mechi za Ligi Kuu za kuanzia Jumapili na Arsenal pia mechi za Portsmouth, Aston Villa na Everton lakini ataiwahi Fainali ya Carling na Aston Villa Februari 28.
Tottenham wamyakua Gudjohnsen kwa mkopo
Meneja wa Tottenham Harry Redknapp amesema Klabu yake imemchukua kwa mkopo Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea na Barcelona Eidur Gudjohnsen hadi mwishoni mwa msimu.
Gudjohnsen kwa sasa ametokea Klabu ya Ufaransa Monaco.
West Ham pia walikuwa wakimuwania Mchezaji huyo mwenye miaka 31 lakini inaelekea wameshindwa kumpata.
Tottenham wanao Mastraika wanne akina Jermain Defoe, Peter Crouch, Robbie Keane na Roman Pavlyuchenko ingawa Pavlyuchenko yuko mguu nje mguu ndani kwani kuna minong’ono huenda akahama.
Gudjohnsen alipokuwa Chelsea walitwaa Ubingwa wa Ligi Kuu mara 2 mwaka 2005 na 2006 na huko Barcelona aliweza kutwaa Mataji manne makubwa mwaka jana yakiwemo ya La Liga na UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Tosic wa Man United yuko FC Cologne
Manchester United wamemkopesha Winga wao kutoka Serbia Zoran Tosic kwa Klabu ya Ujerumani FC Cologne hadi mwishoni mwa msimu.
Winga huyo mwenye umri wa miaka 22 alijiunga na Man United miezi 12 iliyokwisha akitokea Partizan Belgrade lakini amemudu kuchezea mechi 2 tu za Kombe la Carling dhidi ya Barnsley na Tottenham.
Tosic amesema: “Siamini kama huu ndio mwisho wangu Man U!! Nikicheza vizuri Cologne ntarudi tu Old Trafford!!”

No comments:

Powered By Blogger