Friday 29 January 2010

Mafarao Fainali, Algeria wakikwaa kipondo!
• Misri 4 Algeria 0
• Algeria mtu 8 uwanjani baada ya Nyekundu kutembea!!!
Mbele ya Mamia ya Mashabiki wao walioruka na Ndege maalum kwenda Benguela, Angola kutoka Algeria na Misri na kufurika Uwanjani, Misri waliishushia kipigo kitakatifu Algeria cha bao 4-0 na kulipiza kisasi cha kutolewa na Algeria kushiriki Fainali za Kombe la Dunia, kipigo kilichowaacha Algeria wakisambaratika na kubaki mtu 8 tu uwanjani baada ya Wachezaji wao watatu kula Kadi Nyekundu.
Misri watacheza Fainali yao ya 3 mfululizo hapo Jumapili kwa kukutana na Ghana waliyoibwaga Nigeria 1-0 kwenye Nusu Fainali ya awali.
Kiama cha Algeria kilianzia pale Hosni Abd Rabou kufunga kwa penalti baada ya Mchezaji wa Algeria Rafik Halliche kucheza rafu ndani ya boksi iliyompa Kadi yake ya pili ya Njano na hivyo kuwashwa Nyekundu.
Mohamed Zidan alipachika bao la pili, Mohamed Abdelshafi alifunga bao la 3 na Mchezaji hodari wa Akiba, Gedo, kama kawaida yake, alifunga bao la 4.
Baadae kwenye mechi hiyo Wachezaji wa Algeria, Nadir Belhadj na Kipa Fawzi Chaouchi, walipewa Kadi Nyekundu.
Baada ya mechi Kocha Msaidizi wa Misri, Shawki Gharib, alisema: “Tunastahili kuwa Fainali! Tumezifunga timu 3 [Nigeria, Ivory Coast na Algeria] ambazo ziko Fainali Kombe la Dunia!”
Kocha wa Algeria Rabah Saadane alimlaumu Refa Codjia kutoka Benin kwa kipigo chao kwa kusema: “Refa alimpa Kadi Nyekundu Halliche ambae ni Mlinzi wetu bora kwa kosa lilsilostahili! Halafu tulicheza mtu 8 na haiwezekani kwa Timu bora kama Misri!”
Vikosi vilikuwa:
Algeria: Chaouchi, Yahia, Bougherra, Halliche, Belhadj, Yebda, Mansouri, Matmour (Abdoun dakika ya 75), Ziani, Meghni (Laifaoui dakika 67), Ghezzal (Zemmamouche dakika 89).
Akiba hawakucheza: Gaouaoui, Bezzaz, Lemmouchia, Saifi, Raho, Babouche, Zaoui, Bouazza, Ziaya.
Kadi Nyekundu: Halliche (dakika 38), Belhadj (dakika 70), Chaouchi (dakika 88).
Misri: El Hadari, El Mohamady, Gomaa, Fathallah (Gedo dak 59), Moawad (Abdelshafy dak 78), Hassan, Fathi, Said, Abd Rabou, Zidan, Moteab (Ghaly dak 52).
Akiba hawakucheza: Abdoul-Saoud, Salem, El Sakka, Eid, Tawfik, Shikabala, Raouf, Hamdy, Wahid.
Mabao: Abd Rabou dakika ya 39, Zidan dakika 65, Abdelshafy dakika 81, Gedo dakika 90.
Refa: Bonaventure Koffi Codjia (Benin).
Ghana 1 Nigeria 0
  • Nyota Nyeusi Fainali!!  
Bao la Mshambuliaji Asamoah Gyan dakika ya 21 limeiingiza Ghana Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuipiga Nigeria 1-0 hapo jana.
Gyan pia ndie aliefunga bao 1 na la ushindi Ghana walipowatoa Wenyeji Angola kwenye Robo Fainali.
Lakini shujaa wa Ghana aliehakikisha wanatinga Fainali bila shaka ni defensi yao hasa Kipa Richard Kingson waliookoa mikikimikiki yote ya akina Martins, Odemwingie, Obasi, Mikel na wenzao.
Baada ya mechi Mshindi Gyan alisema: “Inashangaza!! Sisi ni Timu ya Vijana Chipukizi na wengi hawakutegemea tutatinga Fainali!”
Vikosi vilikuwa:
Ghana: Kingson, Inkoom, Vorsah, Addy, Sarpei (Rahim Ayew dakika 53), Andre Ayew, Agyemang-Badu, Annan, Asamoah, Gyan (Amoah 84), Opoku (Draman 35).
Akiba hawakucheza: McCarthy, Osei, Mensah, Essien, Narry, Addo, Adiyah, Afful, Adjei.
Nigeria: Enyeama, Mohammed (Odiah 80), Nwaneri, Shittu, Echiejile, Kaita, Mikel, Yussuf (Obinna 67), Odemwingie (Yakubu 70), Martins, Obasi.
Akiba hawakucheza: Ejide, Yobo, Taiwo, Kanu, Olofinjana, Uche, Etuhu, Apam, Aiyenugbu.
Refa: Daniel Bennet (South Africa).
Robinho arudi kwao Brazil!!!
• Yupo Santos kwa mkopo!!
Mchezaji kutoka Brazil, Robinho, ambae kukaa kwake Manchester City kumetawaliwa na majonzi binafsi ya kutokuwa na furaha, yuko mbioni kurudi kwao Brazil kuichezea Santos kwa mkopo wa miezi 6.
Robinho, miaka 26, aliigharimu Manchester City Pauni Milioni 32 walipomnunua kutoka Real Madrid mwaka 2008 ikiwa ni rekodi kwa Uingereza, amekuwa hana namba Man City kwa kuwa kiwango chake kimeporomoka mno na mwenyewe amekuwa akililia aondoke ili kunusuru nafasi yake kwenye Timu ya Taifa ya Brazil itakayocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwezi Juni.
Robinho alikuwa Mchezaji wa Santos kabla kuhamia Real Madrid mwaka 2003.
Man U yamthibitisha Smalling
Manchester United imethibitisha kuwa Difenda Chris Smalling, miaka 20, kutoka Fulham amefaulu vipimo vya afya na amesaini mkataba wa miaka minne ingawa atabaki Fulham hadi mwisho wa msimu huu na kujiunga Old Trafford mwezi Julai.
Smalling, anaechezea Timu ya Taifa ya England ya Vijana chini ya miaka 21, ameshaichezea Fulham mechi 9 msimu huu na Sir Alex Ferguson amezungumza: “Ni mwepesi na anausoma mchezo vizuri. Tumefurahi kumchukua!”
Smalling alitoa shukrani zake kwa Meneja wake Roy Hodgson wa Fulham na kusema: “Nimejifunza mengi Fulham na nawashkuru! Kuja kwenye Klabu bora duniani ni nafasi adimu na nina furaha kubwa!”

No comments:

Powered By Blogger